Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Bei Zapanda kibondo
Bei Zapanda kibondo
By Prosper Kwigize | Published  07/4/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Mwandishi wa HabariTanzania.com, Kibondo
Wakazi wa wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma wamelalamikia kupanda kwa bei ya Nyama pamoja na sigara.
 
Wakiongea na mtandao wa HabariTanzania.com baadhi ya wakazi wa mji wa Kibondo wamebainisha kuwa bei ya nyama imepanda kwa asilimia 70 ambapo kilo moja ya nyama inauzwa shilingi 2000 hadi 2500.
 
Aidha wameeleza kuwa bei ya sigara nayo imepanda kutoka shilingi 50 hadi 80 hali ambayo inasababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa bidhaa hiyo.
 
Akiongea na wanadishi wa habari mmoja wa wamiliki wa maduka ya kuuzia nyama mjini humo Bw. Bangirimana Emanuel amesema kupanda kwa bei hiyo kumetokana na kupanda kwa bei ya ng’ombe minadani.
 
Bw. Emanuel amefafanua kuwa wilaya ya Kibondo haina Ng’ombe wa kutosha kwa ajili ya nyama na badala yake wafanyabiashara hununua ng’ombe hao kutoka wilaya Bukombe na Geita.
 
Amebainisha kuwa bei ya ng’ombe kwa sasa mnadani ni shilingi laki mbili hadi tatu badala ya shilingi laki moja na nusu bei ya awali.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Is Tanzania a safe place to invest?
  4. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Linda Garner
  4. Nthelezi Nesaa
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.