Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Kiingilio kikwazo Sabasaba
Kiingilio kikwazo Sabasaba
By Habari Tanzania | Published  07/3/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Martin Malera

MAONYESHO ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam, yamedorora kutokana na wananchi wachache kujitokeza.

Kudorora kwa maonyesho hayo kulionekana dhahiri juzi na jana, kwani licha ya kuwa siku za mapumziko, wananchi wachache ndio waliotembelea maonyesho hayo.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umebaini kuwa kudorora kwa  maonyesho hayo kumechangiwa na kiingilio kuwa kikubwa.

Mwaka huu watu wazima wanalipa sh 2,000 na watoto sh 1,000, kiwango ambacho kinadaiwa kuchangia kuwapo mahudhurio hafifu, tofauti na miaka iliyopita.

Baadhi ya wananchi waliozungumza na Tanzania Daima, walisema viwango  vya kuingia kwenye maonyesho hayo ni kikwazo kwa wengi.

“Wapo wanaokuja Sabasaba kutafuta bidhaa, ingawa kundi la aina hii ni wachache, lakini lipo kundi kubwa linalokuja Sabasaba kwa ajili ya kutembea na familia.

Ukipanda daladala, nauli  juu, kuingia getini, bei juu, ndiyo maana wanaojitokeza ni wachache,” alisema Fadhili Abdallah.

Kwa upande wa wafanyabiashara, baadhi yao wamelalamikia kodi kubwa tofauti na miaka iliyopita.

Mmoja wa wafanyabiashara ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe, alisema mwaka huu haoni faida ya kushiriki maonyesho hayo, kwani wanunuzi ni wachache na kodi wanayolipa ni kubwa.

Mfanyabiashara huyo aliitaka Bodi ya Biashara ya Nje (BET), ipunguze kodi na kiingilio siku zilizobaki na siku ya kilele, ili wananchi wengi waingie na kufanya manunuzi ya bidhaa


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.