Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Majambazi Wavamia Kambi Ya Wakimbizi Na Kupora Mali Na Fedha
Majambazi Wavamia Kambi Ya Wakimbizi Na Kupora Mali Na Fedha
By Prosper Kwigize | Published  07/3/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Kibondo

Watu wanaodhaniwa kuwa majambazi wamevamia na kupora fedha tasilimu shilingi laki tatu na nusu pamoja na vitu mbalimbali katika kambi ya Kanemba wilayani Kibondo.

Mratibu msaidizi wa Polisi wilayani humo Japheth Kibona amesema kuwa tukio hilo limetokea jana majira ya saa mbili na nusu kwa Bw Barakanfitie Adelino anaeishi Block I kambini humo.

Vitu vingine vilivyoibwa ni pamoja na Radio mbili zenye thamani ya shilingi elfu 22, shuka mbili, suruali mbili aina ya Jinzi, viatu pea mbili na Blanket.

Katika tukio hilo hakuna mtu aliyejeruhiwa kwani Bw Barakanfitie na mkewe walifanikiwa kukimbia na kuwaacha majambazi hayo yakiendelea na uporaji.

Habari kutoka kambini humo zinaeleza kuwa tukio hilo la uporaji lilifanyika katika kipindi cha nusu saa huku majambazi hayo yakiendelea kurusha risasi hewani.

Mrakibu Msaidizi wa polisi wilayani Kibondo amesema hadi sasa hakuna watu wanoshikiliwa kutokana na tukio hilo lakini akabainisha kuwa juhudi za kuwasaka watu hao zinaendelea.
 


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Is Tanzania a safe place to invest?
  4. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Linda Garner
  4. Nthelezi Nesaa
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.