Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Uchumi  »   Wasomi wamtaka JK kukaza buti kwa mafisadi
Wasomi wamtaka JK kukaza buti kwa mafisadi
By Habari Tanzania | Published  01/12/2008 | Uchumi | Rating:
WASOMI wamemtaka Rais Jakaya Kikwete kusimamia kwa ukali na umakini mkubwa ili kuhakikisha watu walioshiriki katika ufisadi uliokithiri katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wanarudisha fedha zote zilizoibwa na wahusika kuchukuliwa hatua.

Hayo yalisemwa jana na Rais wa Serikali ya Wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO), Deo Daudi, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Alisema kuwa utekelezaji wa suala hilo utaliletea heshima taifa katika mapambano dhidi ya rushwa.

Rais huyo wa Daruso alisema kuwa, aliyekuwa Gavana wa BoT, Dk. Daudi Balali na wenzake kutokomeza zaidi ya sh bilioni 133 ni dhambi.

Alisema kuwa wizi wa kiasi hicho cha fedha ni sawa na kubomoa vituo vyote vya afya Tanzania, au kuiba fedha za kuwasomesha wanafunzi wote wa elimu ya juu ndani na nje ya nchi kwa miaka kadhaa.

“Tunampongeza Rais Kikwete tukiamini sasa ameamua kushughulikia suala hili la rushwa bila kusimama, kwa maana hii ndiyo njia pekee ya kuwanasua Watanzania kutoka katika lindi la umaskini ambao wengi tunaona ni wa kuaminishwa zaidi ili kuwapisha akina Balali kutuibia,” alisema Daudi.

Alisema ufisadi haupo BoT pekee na kumtaka Rais Kikwete kugeukia kwenye taasisi nyingine pia.

“Tunamtaka rais aongeze kasi ya kupambana na watu hawa ambao wana dhambi kubwa isiyosameheka ya kuwafanya Watanzania kuwa maskini wa kutupwa katikati ya utajiri uliopindukia,” alisema rais huyo wa Daruso.

Pia alimkumbusha Rais Kikwete na kumtaka kuutambua mchango wa vyombo vya habari katika vita dhidi ya ufisadi na rushwa.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Favourites' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Linda Garner
  4. Marshy Abdu
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.