Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Balali ajiuzulu huku soo la ufisadi BOT likiendelea
Balali ajiuzulu huku soo la ufisadi BOT likiendelea
By Marshy Abdu | Published  12/21/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
Balali ajiuzulu huku soo la ufisadi BOT likiendelea
Na Mwandishi Wetu, Jijini

Wakati sakata la tuhuma za ufisadi katika Benki Kuu nchini, BOT, likiendelea kuzizima, zimepatikana habari kuwa Gavana wa benki hiyo ameandika barua kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Jakaya Kikwete, akiomba kujiuzulu.

Taarifa hizo, ambazo zimeelezwa na chanzo chetu ndani ya Serikali, zinasema kwamba Gavana Balali, ambaye kwa miezi zaidi ya mitatu sasa amekuwa akiendelea na matibabu nchini Marekani, ameandika barua ya kuomba kuachia ngazi kutokana na sababu za kiafya.

``Amemuandikia barua Rais akiomba kujiuzulu kutokana na hali ya afya yake... sifahamu zaidi ya hilo,`` chanzo chetu hicho kimesema.

Aidha, imedaiwa kuwa Gavana Ballali ameandika barua hiyo ya kuomba kujiuzulu siku ya Jumatano.

Hata hivyo, juzi wakati wa mazungumzo yake na waandishi wa habari, Rais Kikwete aliulizwa swali kuhusu madai kwamba Gavana Ballali amekimbia nchi.

Katika majibu yake, Rais Kikwete alisema anachojua yeye ni kwamba Bw. Ballali ni mgonjwa na yuko nchini Marekani kwa matibabu.

Jana, mwandishi wa Alasiri alipomuuliza Waziri wa Fedha Bi. Zakia Meghji kuhusiana na habari hizo za Gavana kuomba kujiuzulu, alikataa kuzithibitisha, akikwepa kukiri wala kuzikanusha.

``Siwezi kukuambia kuwa Balali kajiuzulu ama hajajiuzulu, niliondoka ofisini saa nane Jumatano, lakini hapakuwa na taarifa yoyote,`` akasema.

Kwa miezi kadhaa sasa, wapinzani wamekuwa wakimshutumu Gavana Ballali kuhusika na kile wanachodai kuwa ni ufisadi ndani ya taasisi hiyo nyeti katika uchumi wa nchi, ikiwa ni pamoja na kuidhinisha malipo yenye utata kwa makampuni kadhaa na pia gharama kubwa za ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo Jijini na Zanzibar.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Nthelezi Nesaa
  4. Linda Garner
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.