Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Diwani wa Muhanga atoa wito kunusuru vijana na UKIMWI
Diwani wa Muhanga atoa wito kunusuru vijana na UKIMWI
By Prosper Kwigize | Published  11/16/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
Wito umetolewa kwa serikali na watu binafsi kuwawezesha vijana kujimudu kimaisha ili kuwaepusha na vishawishi vya kijamii ambavyo vitawapelekea kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi
 
 Mheshimiwa Hamis Chubwa, Diwani wa kata ya Muhunga, Kasulu
 
 Wito huo umetolewa na Diwani wa Kata ta Muhunga wilayani Kasulu Bw. Hamis Chubwa wakai akihojiwa na Kigoma yetu juu ya vyanza vinavyochangia kuwepo kwa maambukizi mapya ya virusi vya UKimwi wilayani Kasulu.
 
 Bw. Chubwa amebainisha kuwa kuwepo kwa vijana wanaoshinda vijiweni na katika viambaza vya maduka ya watu wengine bila wao kuingiza chohote pamoja na kupenda starehe za Muziki na sinema ni ishara ya vijana hao kukosa mwelekeo wa kimaisha.
 
 Ametaja kuwa, tabia ya vijana hao kupenda maisha ya hali ya juu bila nyezo kumepelekea kuibuka kwa vijiwe vingi katika maeneo ya masoko ya vijiji na katika barabara kuu ambapo vijana hujadili masuala yasiyo na tija kwao na kutafuta wapenzi.
 
 Aidha amewataka wazazi kuwawekea misingi mizuri ya maisha vijana wao ili wawe na uwezo wa kukabiliana na changamoto za maisha pindi wanapomaliza elimu ya msingi, sekondari na vyuo badala ya kujiingiza katika makubdi ya uharifu na vitendo vya ngono.
 
 Hata hivyo Bw. Chubwa amewataka vijana nao kujitokeza na kujiunga katika vikundi vya akiba na mikopo ambamo anasema wataweza kupata mikopo kutokana na miradi watakayoibua na hatimae kutokomeza utegemezi.
 
 Amewataka pia wanafunzi nao kujibidisha katika masomo yao na kuepuka vitendo vya ngono na kwamba kufanya ngono kwa mwanafunzi huchangia kukwama kimasomo lakini pia kujiongezea nafasi ya kuambukizwa virusi vya ukimwi.
 
 Diwani huyo ambaye licha ya kuwa mwanasiasa, amekuwa akijishughulisha na biashara, pia amewataka wananchi kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu sambamba na kujibidisha katika kazi na michezo kuliko kung’ang’ania anasa za duniani.
 
 Amewataka pia wakazi wa wilaya ya Kasulu kujitokeza kutoa michango ya ujenzi wa mabweni kwa ajili ya wasichana katika shule za sekondari na kuongeza kuwa kundi la wasichana ndilo hasa huathirika na tabia mbaya wawapo shuleni.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Nthelezi Nesaa
  4. Linda Garner
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.