Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Dereva mbaroni kwa kugonga na kuua mara mbili
Dereva mbaroni kwa kugonga na kuua mara mbili
By Prosper Kwigize | Published  11/16/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:
· Aliwahi kuua 2005 hakufikishwa mahakamani
 
 Dreva wa gari la abiria linalofanya safari zake kati ya Kigoma na Kasulu mkoani Kigoma amefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Kasulu mwishoni mwa wiki kwa kosa la kukiuka sheria za usalama barabarani na kusababisha kifo.
 
 Mwendesha mashtaka wa polisi wilayani Kasulu Bw. Rustis Masota amemtaja dreva huyo kuwa ni ramadhan Ahmad mkazi wa Mwanga Mjini Kigoma na kwamba alimgonga na kumuua Bw. Mohdin Ibrahim.
 
 Imeelezwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo tarehe 6 September katika eneo la kijiji cha Kasangezi wilayani Kasulu na kwamba chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi.
 
 Aidha taarifa kutoka jeshi la polisi ambazo zilifikishwa katika mahakama ya wilaya mbele ya hakimu Patrich Ang’ulo zinadai kuwa hilo ni kosa la pili kwa mtuhumiwa huyo ambaye mwaka 2005 aligonga na kuua.
 
 Kwa mujibu wa hati ya mashtaka iliyoambatanishwa na kesi mpya, mshtakiwa Ramadhani alimgonga na kumsababishia kifo Bw. Paschal Kimai mkazi wa kijiji cha Nyumbigwa wilayani humo.
 
 Inadaiwa kuwa mtuhumiwa akiendesha gari lenye namba T 644 AJN mali ya Halfan Soud alikuwa akiendesha kwa mwendo kasi na kumgonga marehemu huyo aliyekuwa akitembea kwa miguu.
 
 Hata hivyo mshtakiwa licha ya kushikiriwa na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani wilayani Kasulu hakufikishwa mahakamani kujibu mashtaka hadi alipokutwa na kosa la pili la September 6 mwaka huu.
 

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Articles to Read' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.