Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Waislamu wataka serikali isitishe uhusiano na Vatican
Waislamu wataka serikali isitishe uhusiano na Vatican
By Marshy Abdu | Published  11/7/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:
Waislamu wataka serikali isitishe uhusiano na Vatican
Wapinga pia ziara ya Papa Benedict XVI

na Dauson Harold


LICHA ya kushinikiza uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi nchini, safari hii viongozi wa dini ya Kiislamu wameibuka na madai mengine, wakitaka serikali ikomeshe mahusiano yake na Vatican.

Wakizungumza katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) jana, viongozi hao waliitaka serikali kufuta mara moja Ubalozi wa Vatican nchini, kwa madai kuwa upo kwa ajili ya Wakristo pekee.

Viongozi hao waliojitambulisha kuwa ni kutoka madhehebu yote yanayounda dini hiyo, walifika MAELEZO na kuzungumza na waandishi wa habari wakiongozwa na Sheikh Mohamed Idd Mohamed wa Msikiti wa Mnyamani, Buguruni.

Sheikh huyo, ambaye alitajwa pia kuwa ni katibu wa kikao cha viongozi wote wa taasisi na dini ya Kiislamu, ndiye aliyesoma tamko kwa niaba ya Mwenyekiti wa kikao kilichoandaa tamko hilo, Alhajj Abbas Sykes.

Katika tamko hilo, viongozi hao walisema kuwa viongozi wa dini ya Kiislamu, maimamu, masheikh na viongozi wa taasisi mbalimbali walikaa kwa pamoja na kujadili mambo mengi yanayohusu dini hiyo.

Katika mkutano huo waliazimia kwa pamoja kutoa tamko la kulikumbusha Bunge na kulitaka lipitie muswada uliowasilishwa na kamati mbili za Katiba na Sheria na kutoa maamuzi yaliyoanishwa.

Pia walikishauri Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuvunja ukimya na kitoe tamko la wazi la kutekelezwa au kutotekelezwa ahadi yake iliyomo katika ibara 108 ya Ilani yake ya uchaguzi kuhusu urejeshwaji wa Mahakama ya Kadhi nchini.

Akitangaza maamuzi mengine yaliyofikiwa katika kikao hicho, Sheikh Mohamed alisema kuwa viongozi hao waliafikiana kufungua kesi dhidi ya Mchungaji Christopher Mtikila, kutokana na matamshi yake yanayoukashfu Uislamu.

Alisema mipango ya kufunguliwa kwa kesi hiyo inakamilishwa kabla kesi yenyewe haijafunguliwa hivi karibuni.

Pia walitumia fursa hiyo kumkumbusha Msajili wa Vyama vya Siasa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Mchungaji Mtikila, ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), kwa kutumia jukwaa la siasa kushambulia dini.

Walimkumbusha pia Rais Jakaya Kikwete kufuta mkataba wa serikali na makanisa kwani itakuwa inakiuka uadilifu, pia walimwomba aufute kwa kuwa una upendeleo wa dini moja dhidi ya dini nyingine.

Pia walimkumbusha rais kuvunja mahusiano kati ya serikali na Ubalozi wa Vatican nchini kwa kuwa Tanzania haifuati dini, kwa hiyo uhusiano wa kibalozi kati ya serikali na Vatican ni kinyume cha katiba ya nchi.

Pamoja na kuitaka serikali kusitisha uhusiano na Vatican, viongozi hao walisema kuwa wanaipinga ziara ya Papa Benedict XVI, aliyepanga kuitembelea Tanzania kutokana na mwaliko wa Rais Kikwete.

Walisema wanaipinga ziara hiyo kutokana na huko nyuma kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki kutoa matamshi ambayo yalielezewa kuwa kashfa kwa Uislamu na Mtume Muhammad (SAW).


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by Omary Shaaban)
    Rating
    There is no reason why we should have Vatican Office here in Tanzania as represent only Minority Christians.
     
  • Comment #2 (Posted by said said)
    Rating
    Pamoja na kuwa mimi nina jina la kiilamu lakini sio mwisilamu.Mimi ni mkiristo jina naomba nieleweke hivyo.
    Maoni yangu kwa waisilamu na wakirisito ni haya:
    1. Kuhusu suala la mahakama ya kadhi waisilamu wasimusumbue mtikila ila waisumbue ccm kwani ndio iliowahidi.Mtikila kuzungumzia suala hilo ni haki yake
    2. Kuhusu suala la Raisi KIkwete kuvunja uhusiano na vatican kwa kuwa ni la kidini hapa naona ni suala la uelewa wa hawa ndugu zetu watanzania. Vatican ni nchi kama ilivyo Irani kuwa ni nchi ya kiisilamu kwa hiyo tanzania tunausiano na Vaticani kama tulivyo na uhusiano na Irani ambayo ni nchi ya kiisilamu. HAPO ISSUE NI UELEWA NIMEMALIZA.
    3. Maoni yangu kuhusu hizi dini mbili yaani uisilamu na ukristo ni kuwa waumini wa dini hizi mbili wasio na fikira na busara ndio waletao machafuko hapa duniani, kwa kuwa wao ndio hujifanya wanamjua sana mungu kuliko watu wengine ndio maana wanatunga na majina, kwa mfano kwa waisilamu mtu asiyekuwa mwisilamu wanamita KAFIRI. wakiristo wanamuita Mpagani. Lakini watu hao hawakasiriki hubaki kucheka tu. Lakini muite muisilamu kuwa yeye ndiye kafiri hapo lazima patachimbika, bora hata wakiristo wanaweza kukuambia kuwa una pepo wa shetani.
    Namliza kwa kusema waisilamu munampeleka mtikila mahakamani atawatoa jashooooooooo!
     
Submit Comment


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Nthelezi Nesaa
  4. Linda Garner
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.