Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Ukodishaji Reli ya Kati matatani
Ukodishaji Reli ya Kati matatani
By Marshy Abdu | Published  10/4/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
Ukodishaji Reli ya Kati matatani
na Mwandishi Wetu


UKODISHAJI wa lililokuwa Shirika la Reli Tanzania (TRC) kwa mwekezaji wa kigeni uliozaa Kampuni mpya ya Tanzania Railway Limited (TRL), unaendelea kukumbwa na matatizo mwanzoni kabisa mwa mkataba wake.

Dosari kubwa inayolikumba shirika hilo ambayo imechukua siku nne sasa ni ile ya wafanyakazi wa TRL wa Dar es Salaam kuwa katika mgomo ambao sasa unaonekana kuendelea kusambaa katika maeneo mengine nchini.

Wafanyakazi hao waliogoma wanadai kulipwa mafao yao kabla hawajahamishiwa kuendelea na kazi chini ya mwekezaji mpya aaliyekabidhiwa uendeshaji wa shirika hilo Jumatatu, katika mkataba wa ukodishwaji wa miaka 25.

Katika kile kinachoashiria kuzidi kuimarika kwa mgomo huo, habari zinaeleza kuwa, umeanza kusambaa sehemu nyingine, kama vile Tabora, ambako inaarifiwa kuwa wafanyakazi wa kitengo cha karakana jana nao walianza kugoma.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, wafanyakazi waliogoma mkoani Dar es Salaam, walisisitiza kuwa wataendelea kugoma hadi hapo watakapolipwa pesa za mkono wa heri kama walivyolipwa baadhi ya wafanyakazi waliokuwa wa Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Habari kutoka ndani ya shirika hilo zimeeleza kuwa, mgomo huo huenda ukaathiri hata safari za treni za abiria ambazo huanzia Dodoma kuelekea Mwanza na Kigoma kupitia Tabora.

“Pamoja na kuwa safari (za abiria) zinaanzia Dodoma, lakini hata njia huko bara nayo si nzuri, iwapo wafanyakazi wataendelea kugoma, inaweza kusababisha hata hizo treni za Dodoma zishindwe kusafiri kwani njia hiyo nayo inahitaji ukarabati wa mara kwa mara,” alisema mfanyakazi mmoja ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini.

Mfanyakazi mwingine aliongeza: “Serikali isifikiri huu ni mchezo, endapo mgomo huu utaendelea, itakuwa ni hatari kwa watu wanaotegemea usafiri wa treni, kwa sababu injini za treni zinazotumika hivi sasa bila kufanyiwa matengenezo kila mara hazifai, sasa mafundi wamegoma, nini kitaendelea hapa... kama si kukwama kwa usafiri.”

Habari zaidi zinaeleza kuwa hali inaweza kuwa mbaya kutokana na kujiingiza katika mgomo huo wafanyakazi wa karakana tatu kubwa za Dar es Salaam, Morogoro na Tabora.

Wafanyakazi hao wameingia kwenye mgomo wakilalamikia kitendo cha baadhi ya wafanyakazi wenzao, kulipwa na Serikali mkono wa heri pamoja na pesa nyingine kwa minajili ya kupunguzwa kazi, lakini wanashangaa kuona wamerudishwa tena kazini Oktoba mosi, wakati TRC inakabidhiwa rasmi kwa mwekezaji mpya, Kampuni ya RITES kutoka India.

Wafanyakazi waliogoma nao wanataka walipwe kama walivyolipwa wenzao, na ndipo waendelee na kazi au waliokwishalipwa wasirudishwe tena kazini.

Hata hivyo, Waziri wa Miundombinu Andrew Chenge, alisema siku ya makabidhiano kuwa suala hilo litapatiwa ufumbuzi kupitia Chama cha Wafanyakazi wa Reli (TRAWU) kwa misingi ya majadiliano.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Nthelezi Nesaa
  4. Linda Garner
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.