Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wananchi waeleza sababu za kumzomea mbunge
Wananchi waeleza sababu za kumzomea mbunge
By Marshy Abdu | Published  08/24/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:
Wananchi waeleza sababu za kumzomea mbunge
na Alli Lityawi, Kahama


WANANCHI wa Kahama, wamesema walimzomea Mbunge wao, James Lembeli (CCM), kwa kuwa alishindwa kuzungumzia sakata la utiaji saini mkataba wa uchimbaji wa dhahabu wa Buzwagi, hivyo kukosa imani kwake.

Wananchi hao wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti jana, walisema kitendo cha mbunge huyo kunyamaza kuhusu suala hilo kimewashitua.

Mbunge huyo alizomewa na wananchi hao alipokuwa akitambulishwa na Rais Jakaya Kiwete ambaye yuko katika ziara ya siku nane mkoani Shinyanga.

Hata hivyo katika mkutano huo, neema ilimuangukia Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige, ambaye alishangiliwa na wananchi hao alipotambulishwa kwa wananchi, ambaye walimfananisha na Mbunge Zitto Kabwe (CHADEMA), wakidai amefanikisha mgogoro wa Kijiiji cha Kakola, ambapo Rais Kikwete aliwahutubia na kuwahakikishia kuwa hawatahamishwa kama ilivyokuwa imeamriwa na serikali hapo awali.

Wakati wakimzomea mbunge wao, wananchi hao walimtaka Rais Kikwete kuondoka naye, kwa madai kuwa ameshindwa kuwatetea wananchi wa Buzwagi.

Pia wamedai tangu achaguliwe amewagawa katika makundi baadhi ya wawakilishi wao katika halmashauri yao ya wilaya, hasa madiwani, ambapo amekuwa akishinikiza migogoro iliyokwamisha maendeleo ya wilaya yao na kugombana na watumishi mbalimbali wa idara za Serikali kwa chuki binafsi.

Kuzomewa kwa mbunge huyo kumezua mijadala mbalimbali ikiwemo ya kumkumbatia kigogo mmoja wa CCM mwenye tuhuma mbalimbali za makosa ya jinai.

Lembeli alikaririwa akilalamika kuzomewa kwake na kudai kuwa huenda ni njama zilizoandaliwa, ili kumharibia jina mbele ya rais, kwa kuwa aliposimama tu, mtu mmoja alipiga mluzi na ndipo umati mkubwa ulipoanza kumzomea kwa nguvu.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.