Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mungu ambae ametupa uzima.
Napenda pia kuwashukuru viongozi wetu wa chama na serikali kwa jinsi wanavyowajibika katika kuwatumikia watanzania katika wilaya hii ya Ulanga.
Napenda kutoa masikitiko yangu kwenu ninyi viongozi wetu kwa yale yanayotusibu sisi wananchi wenu tuliowapa dhamana ya kutuongoza. Inawezekana hamfahamu yale yanayotokea katika kata yetu ya Minepa, lakini kwa uchungu mkubwa napenda kusema matendo ya baadhi ya viongozi wa kata yetu yanahujumu uchumi wa taifa letu na haki za binaadam.
kwanza kabisa viongozi wa kata hii hawataki kushughuikia matatizo ya wananchi mpaka wamepewa hela, kwa mfano kuna kesi ya mama mmoja wa kisukuma alibakwa akaambiwa ili swala lake lishughulikiwe inabidi atoe sh 50000.sasa hii ni haki kweli jamani?
Mungu pia ametubariki na swala la kilimo cha umwagiliaji lakini watu wa kamati ya maji wamekuwa kama miungu , wananyanyasa wengine na kuwafanya wasitumie maji aliyotupa Mungu kwa uhuru, mimi nasema hizo ni hujuma katika kampeni za rais za kuleta mapinduzi ya kilimo. Nauliza jamani kwa nini watu wachache waiweke serikali ya kata mfukoni , na wananchi wasitendewe haki.kila mtanzania anayo haki ya kulima na kutmia maji ambayo MUNGU AMETUPA BURE. Ombi langu kwa mkuu wa wilaya, viongozi hawa hawatufai, waonywe, tunomba pia takuru ifike vijijin ili tupewe haki.
kwa leo naomba niishie hapo
Mungu ibariki Tanzania ,mungu ibariki kata ya Minepa.
Ni mimi mwanachi mpenda maendeleo