Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Jamii  »  Kamati yaeleza kutoridhishwa kasi ujenzi daraja la Kigamboni
Kamati yaeleza kutoridhishwa kasi ujenzi daraja la Kigamboni
By Habari Tanzania | Published  08/4/2007 | Jamii | Rating:
na Martin Malera na Rahel Chizoza, Dodoma


KAMATI ya Maendeleo ya Jamii ya Bunge, imesema hairidhishwi na kasi ya serikali katika kushughulikia suala la ujenzi wa daraja la Kigamboni, ambao umeasisiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Akiwasilisha maoni kuhusu hotuba ya makadirio ya Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, mjumbe wa kamati hiyo, Ezekiel Mahige, alisema pamoja na maandalizi ya kutosha yaliyokwishafanywa na NSSF kwa ajili ya mradi huo, kinachohiotajika hivi sasa ni serikali kuruhusu kuanza kwa utekelezaji wake kwa kuuingiza katika mipango yake ya utekelezaji ukiwa ni utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2005.

Kadhalika, kamati hiyo imependekeza mikopo inayotolewa kwa wajasiriamali ielekezwe katika vyama vya kuweka na kukopa (SACCOS), ili kupunguza mzigo wa riba kwa wakopaji ambao ni wazalishaji wadogo.

Alisema kiwango cha riba ya asilimia 10 inayotozwa kwa SACCOS zinazopewa mikopo na benki ya CRDB, wakati benki ikilipa riba ndogo ya asilimia 2 tu si haki na kushauri riba hiyo kugawanywa kwa usawa wa kila upande kulipa asilimia 6.

Kuhusu mgogoro baina ya wafanyakazi na uongozi wa kiwanda cha sukari cha TPC Moshi, kamati hiyo imeishauri serikali kushughulikia suala hilo na kwamba hali ilivyo kwa sasa inaweza kuleta madhara makubwa na kurudisha nyuma kasi ya uwekezaji nchini.

Kamati pia imezungumzia mradi wa ujenzi wa jengo la wamachinga jijini Dar es Salaam na kushauri kufanyika kwa zoezi la kuwatambua mapema wafanyabiashara wadogo kisha kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali kabla ya kupewa nafasi za kufanya kazi zao katika jengo hilo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.