Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Afrika Ngoma yawa gumzo Ujerumani
Afrika Ngoma yawa gumzo Ujerumani
By Habari Tanzania | Published  08/4/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:
na Mwanne Sekuru


BENDI ya muziki wa dansi ya The Afrika Ngoma, ambayo inafanya shughuli zake nchini Ujerumani imezidi kupanda chati na kuwashika raia wa nchi mbalimbali nchini humo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa Tanzania Daima na kiongozi wa bendi hiyo, Ebrahim Makunja ‘Ras Makunja Kichwa Ngumu’, katika shoo waliyoifanya Juni 2, mwaka huu, katika viwanja Altersorfer jijini Humburg, wakati wa Tamasha la Africa Market, bendi hiyo inayoundwa na wanamuziki kutoka nchi mbalimbali, iliwashika vilivyo maelfu ya mashabiki waliohudhuria.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, bendi hiyo inayopiga muziki wa makabila mbalimbali ya Afrika, ilifanikiwa kuwapeleka puta mashabiki.

Baadhi ya wanamuziki waliocha gumzo kwenye tamasha hilo, ni Christian Bokotesa ambaye alitesa kwenye gitaa la solo, Maxime Vayituma aliyeng’ara kwenye drum, sambamba na kijana mdogo wa miaka 18, mwenye asili ya Kizungu, Lars Bernsmann, aliyekuwa akilicharaza gitaa la rhythm.

Kutokana na kung’ara katika onyesho hilo, bendi hiyo ilitangazwa kuwa bora kwa mara nyingine na kuufanya muziki wa Tanzania kuzidi kupendwa nchini humo.

Mmoja wa waandaaji wa tamasha hilo, Niger Asher, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Colour Music, alisema, haijawahi kutokea kwa muziki wa Afrika kuteka nyoyo za mashabiki, katika historia ya maonyesho ya muziki jijini Humburg.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by msema kweli)
    Rating
    Ndugu mwandishi fanya marekebisho ya jina The Ngoma Africa band siyo afrika Ngoma,bendi inawanamziki wengi watanzania sio wapigaji toka nchi mbali mbali.
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.