Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Polisi kudhibiti wizi kwenye ATM
Polisi kudhibiti wizi kwenye ATM
By Habari Tanzania | Published  08/4/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mohammed Mhina, Jeshi la Polisi


JESHI la Polisi nchini limesema kuwa litakabiliana kwa nguvu zake zote na kuwakamata wale wote wanaojihusisha na wizi wa fedha kwenye ATM katika benki mbalimbali nchini.

Kauli hiyo imetolewa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Sydney Mkumbi.

Alisema hivi sasa Jeshi la Polisi kwa kuwatumia makachero wake linatekeleza mpango mkakati wa kukabiliana na wale wote wanaojihusisha na mtandao huo, ili kunusuru uchumi wa nchi.

Aidha, alisema polisi inawashirikisha pia viongozi wa benki mbalimbali zinazotumia mfumo wa ulipaji fedha kwa njia ya ATM, ili kusaidia kuondoa uwezekano wa kutokea tena kwa wizi kama huo.

Alisema viongozi hao pia wametakiwa kudhibiti nyendo za wafanyakazi waliopo na hata waliowahi kufanya kazi katika mabenki hayo ambao walifukuzwa ama kuachishwa kwa makosa yasio ya uaminifu.

Mkumbi alisema kwa vile wezi hao wanazorotesha uchumi wa nchi, Jeshi la Polisi litahakikisha kuwa wale wote wanaojihusisha na wizi huo wanafahamika na kukamatwa, ili kuchukuliwa hatua kali za kisheria, iwe mfano kwa wengine wenye nia na mawazo ya kufanya vitendo hivyo.

Hivi karibuni, Jeshi la Polisi liliwatia nguvuni watu kadhaa wakiwemo raia wa kigeni kwa tuhuma za kuhusika na wizi wa fedha katika moja ya ATM za benki jijini Dar es Salaam na wamefikishwa mahakamani.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.