RAIS Jakaya Kikwete, amemteua Mohamed Muya, kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam jana na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo, ilisema kuwa kabla ya uteuzi huo, Muya alikuwa Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.
Muya anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Solomon Odunga, ambaye amestaafu kazi hivi karibuni baada ya kufikisha umri wa kustaafu.
Wakati huo huo, Rais Kikwete anatarajiwa kulihutubia taifa kesho Agosti mosi, badala ya leo kama ilivyo kawaida yake.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu jana ilisema kuwa hotuba ya rais kwa taifa imeahirishwa kwa siku moja kutokana na vikao vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) vinavyoendelea mjini Dodoma.
Imeelezwa kuwa katika hotuba hiyo atakayoitoa katika Ukumbi wa Kilimani mjini Dodoma, Rais Kikwete anatarajiwa kueleza na kutoa ufafanuzi kuhusu masuala muhimu ambayo yanawagusa wananchi hivi sasa