Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Makani amtaka JK amwondoe Balali
Makani amtaka JK amwondoe Balali
By Marshy Abdu | Published  07/23/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
Makani amtaka JK amwondoe Balali
na Hussein Malekela


ALIYEKUWA Kaimu Gavana wa Benki Kuu na mwanasheria mashuhuri nchini, Bob Makani, amemshauri Rais Jakaya Kikwete kumfuta kazi Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Daud Balali.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Makani alisema kuwa, kuwepo ofisini kwa Balali kutazuia uchunguzi wa haki kufanyika dhidi ya tuhuma zinazoikabili BoT na yeye mwenyewe binafsi.

Alisema kuwa kwa kuwa Balali ametamka wazi kuwa hatojiuzulu, inampasa Rais Kikwete kumfuta kazi ili timu itakayochunguza tuhuma hizo iwe wazi na kutoa ripoti sahihi kuhusu tuhuma zinazomkabili.

Makani alisema Balali anaweza kudhoofisha uchunguzi kwani anao uwezo wa kuwazuia watendaji walio chini yake kuficha nyaraka muhimu na ushahidi, hivyo ni vema uchunguzi ukafanyika bila ya yeye kuwepo madarakani.

Alisema kwamba wakati wa uchunguzi, Balali aitwe ajitetee akiwa tayari ameshajiuzulu.

Makani alisema kuwa hatua hiyo itahakikisha kuwa ukweli kuhusu tuhuma zilizotolewa utajulikana bila kumuathiri Balali na watu wengine.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Articles to Read' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.