Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Jamii  »  Elimu ya Juu yaainisha mikakati
Elimu ya Juu yaainisha mikakati
By Habari Tanzania | Published  07/21/2007 | Jamii | Rating:
na Tamali Vullu, Dodoma


WIZARA ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia, itaongeza idadi ya wanafunzi wa elimu ya juu kutoka 68,029 hadi 75,346 katika mwaka huu wa fedha.

Akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo bungeni jana, Waziri Profesa Peter Msolla, alisema bajeti hiyo kimsingi inazingatia umuhimu wa kukuza rasilimali watu kwa ajili ya maendeleo endelevu, kama msingi wa mkakati wa kupiga vita umasikini.

Alisema sambamba na hilo, kiwango cha mikopo kwa ajili ya chakula na malazi kwa ajili ya wanafunzi, kimeongezwa kutoka sh 3,500 hadi 5,000 kwa siku.

Aidha, alisema katika mwaka huu wa fedha, serikali itadhamini wanafunzi 1,772 wa shahada ya kwanza ya udaktari (MD), kati ya hao 50 ni wa udaktari wa meno (DDS) katika vyuo vikuu vitano vya sayansi ya afya nchini.

Pia watadhamini wanafunzi 90 raia wa Uganda katika utaratibu wa kubadilishana wanafunzi wa shahada ya kwanza katika vyuo vikuu vya Afrika Mashariki.

Kuhusu suala la mikopo kwa ujumla, Profesa Msolla alisema Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, inatarajia kutoa mikopo katika viwango kati ya asilimia 0 na 100, kulingana na uwezo wa kiuchumi wa kila mwombaji katika ada, elimu kwa vitendo na mahitaji maalum ya vitivo.

Alisema katika kuondoa tatizo la uhaba wa watumishi katika bodi hiyo, wataajiri wafanyakazi 33 wa uchambuzi na utoaji mikopo na kuongeza kasi ya kukusanya madeni kutoka kwa waliokopa kuanzia mwaka 1994.

Waziri huyo alisema hadi sasa wadaiwa 113,240 wametambuliwa na kiasi kinachodaiwa ni sh 51,103,685,914 na kiasi kilichokusanywa hadi Juni mwaka huu ni sh 53,616,011.22.

Aidha, alisema wizara itaongeza idadi ya rasilimali watu kwa kuongeza wataalamu wa kutoa mikopo kwa wanafunzi waliofaulu katika daraja la pili wavulana na wanaochukua masomo ya sayansi.

Kuhusu Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), alisema kilianzisha majaribio ya kutumia panya buku kutambua kuwepo kwa vimelea vya ugonjwa wa kifua kikuu (TB) pamoja na panya hao kuendelea kutumika katika kufichua mabomu.

Alisema matokeo ya awali yameonyesha kuwa, panya buku wana uwezo mkubwa wa kutambua TB kwa kunusa makohozi ya wagonjwa kwa kasi zaidi kuliko binadamu anapotumia hadubini.

Kwa upande wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, katika kipindi cha mwaka huu wa fedha, wizara itakamilisha ujenzi wa awamu ya kwanza ya mradi wa Mlimani City.

Kuhusu Chuo Kikuu cha Dodoma, alisema wizara imetenga nafasi za kazi kwa ajili ya wanataaluma 80 na waendeshaji 134. Pia kimetangaza nafasi za masomo katika fani za elimu, sayansi ya jamii na sayansi za kompyuta.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.