Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Profesa kizimbani kwa kutishia kuua
Profesa kizimbani kwa kutishia kuua
By Habari Tanzania | Published  07/12/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Peter Edson

MHADHIRI Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Haidary Amani, amefikishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kinondoni kujibu shitaka la kutishia kuua.

Akisoma hati ya mashitaka mbele ya hakimu wa mahakama hiyo. Nyigilile Mwaseba, Mwendesha Mashtaka, Inspekta Benedict Nyagabona, alidai mshitakiwa, ambaye ni mkazi wa Kawe, alifanya tukio hilo Juni 30.

Alidai mtuhumiwa alitishia kwa kumpigia simu mlalamikaji Kuluthum Ahmad kuwa atampoteza, akimaanisha kuwa atamuua, kitendo ambacho ni kinyume cha sheria.

Hata hivyo Inspekta Nyagabona alidai kuwa bado haijafahamika chanzo cha ugomvi kati ya mlalamikaji na mtuhumiwa na kwamba upelelezi dhidi ya kesi hiyo unaendelea.

Mtuhumiwa alikana shitaka hilo na kupewa dhamana baada ya kusaini bodi ya Sh300,000 hadi Agosti 30, kesi hiyo itakapotajwa.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.