Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Amuua mamaye msibani
Amuua mamaye msibani
By Habari Tanzania | Published  07/7/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Shangwe Thani, Shinyanga


MKAZI wa Kijiji cha Mwamalili, wilayani Shinyanga, Mande Manyanya (22), anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi akiwa msibani.

Manyanya, anadaiwa kumuua mama yake, Wande Bulungu (60) kwa kutumia mapanga. Mama huyo alikuwa kwenye msiba wa mama yake mzazi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Shaibu Ibrahimu, alisema Manyanya alimuua mama yake kwa kumtuhumu kumfunga uzazi mkewe. Tukio hilo lilitokea Julai mosi mwaka huu, saa moja usiku katika Kijiji cha Ihapa, Wilaya ya Shinyanga.

Alisema tukio hilo lilitokea wakati mama huyo akiwa amelala na wanawake wengine nje ya nyumba iliyokuwa na msiba.

“Katika shambulio hilo, Wande alikatwakatwa kwa mapanga na kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili wake… alikimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga alikolazwa na siku iliyofuata alifariki dunia,” alieleza kamanda huyo wa polisi na kuongeza kuwa, muuaji huyo yupo mikononi mwa polisi.

Kamanda Shaibu alieleza kuwa, baada ya kuhojiwa na polisi, mtuhumiwa alikiri kuhusika na mauaji hayo, akidai kuwa mama yake alimloga mke wake kwa kumfunga kizazi.

Alisema kuwa mtuhumiwa huyo alisema mama yake huyo pia alisababisha kuvunjika kwa ndoa ya dada yake kwa mumewe.

Alidai, katika maelezo ya mtuhumiwa huyo kwa polisi, alisema mpango wa mauaji hayo ulifanywa kwa ushirikiano na shemeji yake aliyemlipa sh 10,000 na panga, ili akamilishe azma ya kumuua mama huyo kwa imani za kishirikina.

Kamanda huyo, alisema polisi inaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.