Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Uchumi  »  Kombani atoa agizo kwa halmashauri
Kombani atoa agizo kwa halmashauri
By Habari Tanzania | Published  07/6/2007 | Uchumi | Unrated
na Peter Nyanje na Rachel Chizoza, Dodoma


NAIBU Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Celina Kombani, ameziagiza halmashauri ambazo bado hazijatekeleza agizo la kutoa asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya mifuko ya mikopo kwa vijana na wanawake zifanye hivyo mara moja na kumpelekea taarifa za utekelezaji ofisini kwake kila baada ya miezi mitatu.

Alitoa agizo hilo baada ya kubainisha kuwa takwimu za mwaka 2005/06 zinaonyesha kuwaa halmashauri nyingi zilikuwa hazijatekeleza agizo hilo. Alisema halmashauri 36 kutoka mikoa 16 nchini hazikuchangia kabisa mfuko huo na halmashauri 15 kutoka mikoa tisa zilichangia kiasi kidogo.

“Kwa mara nyingine, naziagiza halmashauri ambazo hazijachangia kikamilifu kutekeleza agizo hilo la kutenga asilimia kumi ya mapato yake kwa ajili ya mifuko ya wanawake na vijana,” alisema wakati akijibu swali la Mbunge wa Koani, Haroub Masoud (CCM).

Aidha, Kombani alivitaka vikundi mbalimbali vya vijana na wanawake, vilivyokopa fedha kutoka katika mifuko hiyo kurejesha mikopo hiyo, ili na wenzao nao wapate fursa ya kukopa.

Alizitaka halmashauri ambazo zilifanya vizuri katika kuchangia mifuko hiyo kuwa ni Manispaa za Ilala, Morogoro, na Kinondoni, majiji ya Mbeya na Dar es Salaam pamoja na Wilaya za Bukombe, Kwimba, Mbeya, Kashama na Kilombero.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Nthelezi Nesaa
  4. Linda Garner
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.