Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Kikwete akerwa na walinzi wake
Kikwete akerwa na walinzi wake
By Marshy Abdu | Published  07/4/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:
Kikwete akerwa na walinzi wake
na Ratifa Baranyikwa


RAIS Jakaya Kikwete jana alilazimika kuingilia kati na kuwataka walinzi wake waache kuwabughudhi wapiga picha ambao walikwenda kutekeleza majukumu yao katika mapokezi ya Rais wa Msumbiji, Armando Guebuza.

Rais alichukua hatua hiyo baada ya kushuhudia wapiga picha wakisukumwa na kutakiwa kusimama mbali na eneo la tukio jambo ambalo lingewafanya washindwe kupata picha nzuri za mapokezi ya kiongozi huyo wa Msumbiji.

Rais Kikwete ambaye alikuwa akifutilia tukio hilo kwa muda, wakati anasubiri mwenyeji wake ateremke katika ndege iliyomleta, aliwaamuru maofisa hao waache kufanya hivyo lakini mmoja kati yao hakuonekana kuelewa.

“Wee njoo hapa.....” alimuita ofisa aliyekuwa anaongoza operesheni hiyo na kumuuliza kwanini anawazuia wapiga picha kufanya kazi yao.

“Acha watu wafanyekazi yao, kwanini unawazuia?” alihoji Rais na kumfanya ofisa huyo na walinzi wake wengine kujiweka pembeni na kuwaacha wapiga picha watekeleze wajibu wao.

Hali hiyo ilionekana kuwapa faraja wapiga picha ambao walisema kwa nyakati tofauti kuwa maofisa hao wamekuwa na tabia ya kuwasukuma bila sababu za msingi na wakati mwingine kuhatarisha vitendea kazi vyao.

Rais Guebuza akiwa nchini atakutana na wanajamii wa Msumbiji waliopo nchini kabla ya kufungua Maonyesho ya 31 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam na jana alikuwa na mazungumzo na mwenyeji wake.

Rais Kikwete aliwasili uwanja wa ndege akitokea nchini Ghana na kumsubiri mgeni wake, na waliondoka wote hadi Ikulu.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Articles to Read' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.