Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Makamba kavuruga mambo Z’bar - CUF
Makamba kavuruga mambo Z’bar - CUF
By Habari Tanzania | Published  06/12/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu


CHAMA cha Wananchi (CUF), kimesema kauli iliyotolewa hivi karibuni kisiwani Pemba na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Luteni Yusuf Makamba, imeharibu na kuchafua hali ya hewa kisiasa Visiwani Zanzibar.

CUF pia imesema kufuatia kauli hiyo ya Makamba, itachukua muda mrefu zaidi kurejesha katika ya hali ya kawaida mazungumzo yanayoendelea baina yake na CCM.

Kauli hiyo ilitolewa na kiongozi wa CUF katika mazungumzo hayo, ambaye pia ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Hamad Rashid, wakati alipozungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki.

Rashid alikuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi aliyetaka kujua mchakato wa kisiasa unaoendelea visiwani Zanzibar na hali ya mambo baada ya ziara ya Makamba kisiwani Pemba, hivi karibuni.

“Kwa kweli wanachama wetu wamesikitishwa na kauli ya Katibu Mkuu wa CCM, na wameleta maoni yao kuwa CUF ijitoe katika mazungumzo yanayoendelea,” alisema Rashid.

Rashid aliongeza kwamba, CUF imejitahidi kutuliza munkari wa wanachama wake kwa kuwataka wavute subira, na kuwaamini kwamba ni viongozi wao wanaostahili kusikilizwa.

Alisema kimsingi, ziara ya Makamba huko Pemba, mwezi uliopita haikuwa na maana kwani haikueleza kile ambacho wananchi walitarajia katika mazungumzo yanayoendelea, badala yake alitumia muda wake mrefu kuibeza CUF na kutengeneza fitina.

Kwa msingi huo, Rashidi alisema kwamba CUF bado inaamini umuhimu wa kuwapo kwa mchakato wa mazungumzo hayo, hivyo iliwasiliana na CCM kujua kinachoendelea na matamshi ya Makamba.

“Kama ni kujitoa katika mazungumzo ni maamuzi yanayopaswa kuamuliwa na Baraza Kuu la Uongozi la CUF, na lolote linaweza kutokea, ama kuendelea na mazungumzo ama kujitoa,” alisema Rashid.

Alisema yeye binafsi kama mbunge kutoka Pemba, kiongozi mwandamizi wa CUF na sehemu ya mazungumzo hayo, hakubaliani na kauli za Makamba, na kushindwa kuamini kama zinaweza kutolewa na kiongozi mkubwa kama yeye.

“Lakini tunadhani hiyo ndiyo rangi ya CCM, na sisi mara zote tupo makini kusikiliza wao wanasema nini, lakini kwa hili tunadhani (Makamba) amekurupuka kutoa kauli bila kufanya utafiti.

“Kauli zake hazionyeshi ukomavu na nia ya wazi ya CCM kama chama kinachotawala nchi, kushughulikia mgogoro wa kisiasa huko Zanzibar, lakini pia wanachama wetu wanaamini alifanya ziara ile kwa lengo la kubomoa,” alisema.

Hata hivyo, Rashid alisema kwamba CUF haijapata athari zozote baada ya ziara hiyo, kama ambavyo yeye mwenyewe Makamba alivyoueleza umma kuwa amefanikiwa kukisambaratisha chama cha CUF.

“Makamba baada ya kurejea katika ziara ya Zanzibar, alisema kwamba amekivuruga chama cha CUF Pemba na kuiteka nyara ngome yetu, sisi hatujaona hilo, lakini mashaka yetu ni matamshi, kama yana nia gani katika mazungumzo yanayoendelea.

“CUF ni chama imara, hatuna tatizo kabisa, tunajua kile tunachokifanya na wala maneno ya Makamba hayatutishi, shida yetu ni je, huo ndio msimamo wa CCM?” alihoji.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.