Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wakubwa wadaiwa mamilioni Ilala
Wakubwa wadaiwa mamilioni Ilala
By Marshy Abdu | Published  05/23/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
Wakubwa wadaiwa mamilioni Ilala
na Lucy Ngowi


HALMASHAURI ya Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam, imetoa notisi kwa wadaiwa sugu wa kodi za majengo wilayani humo, na kuwapa muda walipe deni hilo kabla hatua kali za kisheria hazijachukuliwa dhidi yao.

Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na halmashauri hiyo, wadaiwa hao sugu 49, wamelimbikiza madeni ya karibu sh milioni 308.

Miongoni mwa watu wanaodaiwa ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Salum Londa, ambaye anadaiwa sh 1,793,668.

Ofisa Habari wa Manispaa hiyo, Lucy Semindu, alipozungumza na Tanzania Daima jana, alisema iwapo mpaka Juni 30 mwaka huu wadaiwa hao watakuwa hawajalipa madeni hayo, wanatarajiwa kufikishwa mahakamani.

Kwa mujibu wa Semindu, halmashauri hiyo imekuwa ikiwafuatilia wadaiwa hao na baadhi yao wameweza kulipa, baadhi ya fedha wanazodaiwa.

Alisema endapo wadaiwa hao sugu hawatalipa, manispaa inakusudia kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria ya kodi ya majengo na. 2 ya mwaka 1983 na sheria ndogo ya kodi ya majengo ya halmashauri hiyo ya mwaka 2003.

“Manispaa inakusudia kuwafikisha mahakamani endapo hawatalipa madeni hayo. Imetoa muda mpaka Juni 30 mwaka huu wawe wameshakamilisha au wanaendelea kulipa,” alisema Semindu.

Mbali na Londa, Semindu aliwataja baadhi ya wadaiwa wengine na fedha wanazodaiwa zikiwa kwenye mabano ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Tiba Muhimbili (MUCHS – sh 12,407,026), Shirika la Msalaba Mwekundu (sh 5,347,856), Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA sh 6,738,823) na Scandinavia Express (sh 3,089,872).

Wengine ni Shirika la Masoko Kariakoo (sh 18,722,726), Tanzania Postal Corporation (sh 29,840,375), Embassy Hotel (sh 14,681,201), Hospitali ya St. Bernard (sh 2,254,418), Masumin Printways (sh 1,271,126) na Chuo cha Ufundi (DIT) (sh 12,520,362).

Wengine ni Shirikisho la Soka Tanzania (TFF sh 1,617,904), Klabu ya Yanga (sh 6,738,823) na Klabu ya Simba (sh 2,944,533).

Ofisa habari huyo alitumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wamiliki wa majengo yote endapo wanakusudia kufanya badiliko la umiliki wa majengo waifahamishe manispaa ili jina liweze kubadilishwa.

Alisema pesa hizo zinazolipwa zinasaidia halmashauri katika kutoa huduma mbalimbali kama ujenzi wa shule, barabara na uzoaji taka.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.