Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Jamii  »  ‘Teknohama kikwazo cha maendeleo’
‘Teknohama kikwazo cha maendeleo’
By Habari Tanzania | Published  05/21/2007 | Jamii | Unrated
na Sitta Tumma, Mwanza


IMEELEZWA kwamba kiwango duni cha elimu kuhusu teknolojia ya mawasiliano ya kisasa (TEKNOHAMA), ni moja ya sababu kubwa zinazofanya vita dhidi ya umaskini na ujinga isifanikwe nchini.

Serikali kupitia Wizara ya Miundombinu, imetakiwa kushirikiana vyema na wadau kutoka sekta mbali mbali za mawasiliano, ili kuboresha na kusambaza huduma hiyo hadi vijijini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa vyama vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Mawasiliano Kanda ya Ziwa (SWOPnet), Abubakar Karsan, aliyasema hayo wakati akizungumza kwenye mdahalo wa mawasiliano uliofanyika jijini hapa.

Mkurugenzi huyo alieleza kuwa kutoboreshwa kwa mawasiliano ya teknolojia ya kisasa, hususan katika sekta za elimu, afya na kilimo, ndiyo sababu kuu inayochangia kudidimiza maendeleo na uchumi nchini.

“Umefika wakati serikali ione umuhimu wa kupeleka kompyuta mashuleni, hospitalini, vituo vya afya na ipeleke mawasiliano hayo vijijini kwa wakulima ili na wao waweze kufanya kazi zao kwa upeo na utandawazi zaidi,” alishauri.

Akifafanua, Karsan ambaye pia ni Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Waandishi mkoani Mwanza (MPC), aliitaka serikali kuona umuhimu wa kubuni mbinu mpya za kukabiliana na lindi la umaskini lililowagubika Watanzania.

Alisema njia pekee ya kuondokana na adha hiyo ni kuwekeza katika teknolojia ya mawasiliano na kwamba ni vyema wananchi wakawezeshwa kwa kuboreshewa mawasiliano hayo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Articles to Read' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.