Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Daruso kujitoa mhanga kuwaokoa wenzao 56
Daruso kujitoa mhanga kuwaokoa wenzao 56
By Habari Tanzania | Published  05/15/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Lucy Ngowi


MARA baada ya kurejea chuoni jana, viongozi wa Serikali ya Wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso), ambao hawajasimamishwa, waliitisha kikao, ambacho moja ya ajenda zake kubwa ni kutafuta namna ya kuwatetea viongozi wenzao waliosimamishwa.

Mmoja wa viongozi wa Daruso ambaye alirejea chuoni jana baada ya msamaha wa jumla, alilithibitishia gazeti hili kuwa, wamepanga kutafuta mbinu za kuwatetea wenzao ili warejeshwe chuoni ‘kwa gharama yoyote ile.’

“Tunaendelea na kikao chetu na hoja kubwa ni kutafuta namna ya kuwarejesha wenzetu chuoni kwa gharama yoyote,” alisema kiongozi huyo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini.

Mmoja wa viongozi wa Daruso aliyesimamishwa alisema kuwa, pamoja na wao kusimamishwa, bado Serikali ya Daruso ipo na Makamu wa Rais wa serikali hiyo, Benadeta Lushahu ndiye anayekaimu nafasi ya rais aliyesimamishwa.

“Makamu wa Rais hajasimamishwa. Serikali ya Daruso ipo na bado wanaweza kukaa vikao vya maamuzi kwa ajili ya kuwatetea wenzao,” alisema.

Tanzania Daima jana ilishuhudia umati wa wanafunzi waliorejea chuoni hapo wakijaza fomu maalum zilizowataka kuahidi kutii masharti yote yaliyowekwa na uongozi wa chuo hicho.

Hata hivyo, katika hali isiyo ya kawaida, Makamu Mkuu wa Chuo, Profesa Rwekaza Mukandala jana alikataa kuzungumza na waandishi wa habari, ambao walitaka kupata maelezo mbalimbali kutoka kwake likiwamo lile linalohusu hatima ya wanafunzi waliosimamishwa.

Pamoja na waandishi wa habari kumweleza nia ya kutaka ufafanuzi huo, Prof. Mukandala alimtuma msaidizi wake na kuwaeleza waandishi wa habari kuwa, taarifa zote zinapatikana katika ofisi ya uhusiano chuoni hapo.

Hata hivyo, Afisa Uhusiano wa chuo hicho, Julius Saule, alipofuatwa, alisema alikuwa hana habari mpya wala hakuwa na lolote la kuzungumza na waandishi.

Waandishi wa habari walipomfuata kwa mara nyingine tena Prof. Mukandala, hakuwa tayari kusema lolote na badala yake akaonekana akichukua mkoba wake na akaondoka na gari yake yenye namba za usajili SU 35959 aina ya Land Cruiser.

“Kwa leo sina la kuzungumza, wala siko tayari kujibu maswali,” alisema Prof. Mukandala huku akiwa anatoka nje ya mlango wake ambapo aliongozana na waandishi wa habari hadi alipoingia kwenye gari lake na kuondoka.

Jumamosi iliyopita, uongozi wa chuo kikuu hicho, ulitangaza uamuzi wake wa kuwarejesha wanafunzi wote wa shahada ya awali waliosimamishwa, isipokuwa wanafunzi 56 ambao wamesimamishwa kwa muda usiojulikana.

Kwa maelezo ya Prof. Mukandala, wanafunzi hao waliosimamishwa, wanatakiwa watoe maelezo zaidi kuhusu kushiriki kwao kwenye mgomo huo, na wale watakaoonekana hawakuwa vinara wa mgomo, ndio watakaoruhusiwa kuendelea na masomo.

Katika kampasi ya Mlimani, wamesimamishwa wanafunzi 22, Chuo Kishiriki cha Ualimu Chang’ombe (DUCE) wanafunzi 11, Chuo Kishiriki cha Ualimu Mkwawa (MUCE) wanafunzi sita na Chuo cha Ardhi na Usanifu wa Majengo (UCLAS) wanafunzi 16.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Articles to Read' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.