Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Exim Bank waanzisha Master Card
Exim Bank waanzisha Master Card
By Habari Tanzania | Published  06/23/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated

BENKI ya Exim, jana ilizindua kadi mpya (Master Card) itakayotumika kuchukulia fedha ndani na nje ya nchi.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Sabetha Mwambenja, alisema mtumiaji wa kadi hiyo ataweza kuitumia hata akiwa nje ya nchi.

Mwambenja alisema wameamua kuanzisha kadi hiyo ili kuwasaidia wateja kutosafiri na fedha nyingi mifukoni wanapokuwa na safari nje ya nchi.

“Tumeamua kwa makusudi kuanzisha huduma hizi kwani zitasaidia wateja kutobeba maburungutu ya fedha ambapo wanaweza kupoteza au hata kuibiwa, lakini ukiwa na kadi si rahisi kuibiwa,” alisema.

Mwambenja alisema wateja watakaohitaji fedha zaidi kwenye akaunti zao kwa kutumia kadi hizi, wataweza kukopeshwa na watakapoingiza fedha zitakatwa kufidia.

Benki hiyo ina jumla ya wateja 80 ambao tayari wanatumia huduma ya kadi hiyo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.