Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Sekta binafsi kutibu Muungano
Sekta binafsi kutibu Muungano
By Habari Tanzania | Published  04/24/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu


BAADA ya muda mrefu wa malumbano na mabishano kuhusu kile kinachoitwa kero za Muungano, serikali sasa imeamua kuishirikisha sekta binafsi ili kuukuza.

Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki iliyopita na Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Shein, wakati alipokuwa anazungumza na jumuiya ya Watanzania wanaoishi Geneva, nchini Uswisi, ambako alikuwa katika ziara ya kiserikali.

Katika mazungumzo hayo, Dk. Shein alisema serikali imebaini kuwa sekta binafsi ina nafasi kubwa katika kukuza ushirikiano baina ya watu wa Tanzania Bara na Zanzibar.

Hivyo, wakati umefika sasa wa kuishirikisha sekta hiyo, kama njia mojawapo ya kuhakikisha kuwa kero za Muuungano zinashughulikiwa.

Chini ya mpango huo wa kuishirikisha sekta binafsi, Dk. Shein alibainisha kuwa, serikali ina mpango wa kuandaa miradi ya kiuchumi ya pamoja itakayoishirikisha sekta binafsi.

Alisema ni matumaini ya serikali kuwa, mipango hiyo ya uchumi, ambayo utekelezaji wake upo mbioni, itasaidia kukuza uchumi wa pande zote mbili za Muungano.

Aidha, Dk. Shein alibainisha kuwa, Serikali ya Muungano na ya Zanzibar, tayari zimeshaanza kuchukua hatua madhubuti katika utekelezaji wa dhamira ya kuondoa kero zote za Muungano kwa lengo la kuimarisha umoja wa kitaifa.

Alibainisha kuwa, katika kufanikisha azma hiyo, Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha, wamekwishakutana mara mbili, katika vikao ambavyo vimefikia maamuzi mbalimbali yanayolenga kutatua kero za Muungano.

Dk Shein aliwaambia Watanzania hao kuwa, mikutano inaonekana kuzaa matunda kwani baadhi ya mambo ambayo yanaonekana kuwa kero katika Muungano, yameanza kupatiwa ufumbuzi wakati masuala mengine yapo katika hatua ya kumalizika.

Aidha, katika hicho Dk. Shein alizungumzia jitihada zilizochukuliwa na serikali katika kukabiliana na changamoto za ujambazi, ukame na magonjwa mbalimbali ikiwemo homa ya bonde ya ufa (RVF), iliyojitokeza nchini mwanzoni mwa mwaka huu pamoja na masuala ya kuimarisha elimu, kilimo na ukusanyaji wa mapato kwa ujumla.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.