Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Barabara Sam Nujoma kujengwa kwa mafungu
Barabara Sam Nujoma kujengwa kwa mafungu
By Habari Tanzania | Published  06/21/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Nasra Abdallah
 
BARABARA ya Sam Nujoma inatarajiwa kutengenezwa kwa vipande vipande kutokana na pingamizi zilizowekwa mahakamani na baadhi ya wakazi waliojenga pembezoni mwa eneo la barabara hiyo.
 
Mhandisi wa Mfumo wa Mawasiliano ya Kompyuta wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Rickson Joseph, alisema hayo juzi, alipozungumza na Tanzania Daima kwenye maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam .
 
“Ukweli ni kwamba katika ujenzi huo kuna baadhi ya nyumba zilizoko kwenye eneo la barabara zinazopaswa kuondolewa na nyingine upanuzi wa barabara unalazimu kuzikumba, na hizo ndizo zina malalamiko mahakamani, hatuwezi kuzibomoa mpaka mahakama itakapotoa uamuzi,” alisema.
 
Joseph alisema barabara hiyo inayotarajiwa kukamilika Juni mwaka 2007, itagharimu sh bilioni 12,973 na itakuwa na njia nne pamoja na njia ya waenda kwa miguu.
 
Barabara hiyo yenye urefu wa km 4 kutoka makutano ya Barabara ya Bagamoyo hadi Ubungo, itajengwa kwa kiwango cha lami na kuwekwa taa za kuongozea magari katika makutano ili kuepuka msongamano wa magari.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.