Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Kawawa awataka wananchi kuwaumbua viongozi wabovu
Kawawa awataka wananchi kuwaumbua viongozi wabovu
By Habari Tanzania | Published  04/2/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Lina Luka, Morogoro


WAZIRI Mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rashid Mfaume Kawawa, amewataka wananchi kupambana na viongozi wa ushirika wanaotumia nyadhifa zao kujitajirisha badala ya kunufaisha walengwa kwa kupatiwa mikopo.

Kawawa alitoa kauli hiyo wakati akiwahutubia waumini wa dini ya Kiislamu kwenye baraza la Maulid lililofanyika kitaifa katika Chuo Kikuu cha Kiislamu, mjini hapa.

“Ushirika si sehemu ya kujitajirisha mtu binafsi, ni mahali pa kujiunga ili kupambana na umaskini,” alisema.

Alisema mara nyingi viongozi wa ushirika wakichaguliwa kushika nafasi mbalimbali, hujenga imani kuwa wamekwishatajirika.

“Viongozi wa aina hii lazima tupambane nao ili kuhakikisha ushirika wetu unadumu na kuwanufaisha wanachama wake,” alisema.

Pia alisema njia pekee ya kupambana na umaskini ni kujiunga katika vikundi vya uzalishaji mali na kutumia fursa za mikopo zinazotolewa na asasi mbalimbali katika kuendeleza miradi itakayowakwamua kiuchumi.

Hata hivyo, Kawawa amewaasa waumini wa dini ya Kiislamu kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shule ili kupata elimu ya kutosha.

Awali akisoma salamu za Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA), Sheikh Ramadhani Sawaka alisema baraza hilo lina watoto yatima 100 ambao wanahitajika kugharamiwa na baraza hilo.

Alisema baraza hilo linahitaji zaidi ya sh milioni 50 ili kufanikisha mahitaji hayo.

Sheikh Sawaka alitoa wito kwa Waislamu nchini pamoja na watu wenye mapenzi mema kwa yatima, kusaidia upatikanaji wa kiasi hicho cha fedhas ili kufanikisha azma hiyo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.