Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wezi wa mafuta ya transfoma ni TANESCO wenyewe - Mbunge
Wezi wa mafuta ya transfoma ni TANESCO wenyewe - Mbunge
By Habari Tanzania | Published  04/2/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Christopher Nyenyembe, Mbeya


MBUNGE wa Mbeya Mjini, Benson Mpesya, amesema wezi wa mafuta ya transfoma za Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ni wafanyakazi wenyewe wa shirika hilo.

Mbunge huyo ameamua kutoboa siri hiyo kutokana na giza nene linaloendelea kuwakumba baadhi ya wakazi wa Jiji la Mbeya kwa zaidi ya miezi miwili kutokana na ongezeko la wizi wa mafuta ya transfoma, huku akiwa mmoja wa waathirika na hali hiyo.

Mpesya anayeishi eneo la Iganzo, amekuwa miongoni mwa wakazi wa jiji wanaolala gizani kutokana na hujuma inayofanywa na wananchi wanaoliibia shirika hilo mafuta hayo na kuziacha transfoma zikilipuka.

Kutokana na wizi huo, Mpesya ameamua kuweka hadharani ukweli wa hujuma hizo kwa kudai kuwa, wanaohusika na njama hizo dhidi ya shirika hilo ni wafanyakazi wenyewe wa TANESCO na si vinginevyo.

Katika mahojiano yake na Tanzania Daima juzi, mbunge huyo ambaye alikuwa mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge iliyokuwa mkoani hapa kukagua shughuli mbalimbali za kiusalama, alisema hakuna mwananchi wa kawaida anayefaya wizi huo isipokuwa ni wafanyakazi wenyewe wa TANESCO.

“Nimepewa taarifa na baadhi ya wananchi kuwa, wanaohusika na wizi huo ni wafanyakazi wa TANESCO na ndio wenye vifaa vya kupanda kwenye nguzo wakiwa na gloves, ngazi za TANESCO na vifaa maalumu vya kufungulia transfoma, hakuna watu wengine,” alisema Mpesya.

Aliyataja maeneo mengine yaliyokumbwa na wizi huo kuwa ni Isanga, Iganzo Tankini na Iganzo kwa Mbunge ambako transfoma tatu zimeibwa mafuta na hivyo kuwafanya wananchi wa maeneo hayo waishi gizani.

Alisema hali ya usalama katika Jiji la Mbeya hivi sasa inatia shaka na kuashiria kuongezeka kwa matukio ya uhalifu, hasa kutokana na giza lililotanda kwenye mitaa kadhaa jijini hapa kutokana na wizi wa mafuta ya transfoma kuzidi kuongezeka.

Mpesya alisema umefika wakati ambao wananchi katika mitaa yao wanapaswa kupewa jukumu la kuzitunza na kuzilinda transfoma hizo na hatakiwi mtu yeyote anayejifanya mfanyakazi wa shirika hilo kupanda kwenye nguzo bila kukutana na uongozi wa mtaa ili wafahamu kitu kinachotakiwa kufanywa.

Pia aliushauri uongozi wa shirika hilo kufanya utafiti wa kina unaohusu matumizi ya mafuta hayo licha ya kuwepo kwa watu wengi wanaodai kuwa yanatumiwa kukaangia chipsi, lakini alielezea wasiwasi wake akidai kuwa inaonekana yana kazi nyingine zaidi na ndiyo maana wizi huo haukomi.

Hivi karibuni, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Mbeya, Deogratias Ndamugoba alisema katika kipindi kifupi, zaidi ya transfoma sita ambazo gharama yake halisi bado haijafahamika, zimeungua kutokana na wizi wa mafuta.

Meneja huyo alisema kutokana na hujuma hiyo, maeneo kadhaa yatakosa umeme kwa muda usiojulikana kutokana na kukosekana kwa transfoma za akiba na kukosa mafuta hayo.

“Hata makao makuu Dar es Salaam tumewasiliana nao hawana transfoma za akiba. Tanzania hatuna mafuta maalumu kwa transfoma, kwa hiyo maeneo mengi yataathirika, wateja waliokuwa wakizitegemea transfoma hizo watakosa huduma ya umeme kwa muda mrefu,” alisema meneja huyo.

Ndamugoba aliwaomba wananchi watoe ushirikiano katika kuwadhibiti wahalifu hao na kwamba mtu yeyote atakayeonekana akijishughulisha kwenye transfoma bila gari la TANESCO, akamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.