Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mugabe aambiwe ukweli
Mugabe aambiwe ukweli
By Habari Tanzania | Published  03/29/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:

MKUTANO wa viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), umeanza jana chini ya Uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete.

Miongoni mwa mambo yanayotarajiwa kuchukua nafasi kubwa kujadiliwa katika mkutano huo, ni migogoro ya kisiasa nchini Zimbabwe na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Macho na masikio ya Waafrika wengi yako jijini Dar es Salaam ambako mkutano huo unafanyika, na kikubwa wanachofuatilia ni nini viongozi wa jumuiya hiyo watamuambia au kumshauri Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, ambaye pia anahudhuria mkutano huo.

Wengi wanataka kusikia viongozi hawa watasema nini kuhusu Zimbabwe na Mugabe, kutokana na matukio ya hivi karibuni ambayo yamevuka mipaka ya kawaida ya ushindani wa kisiasa na hata ubinadamu, yaliyofanywa na vyombo vya dola vya serikali ya Mugabe dhidi ya viongozi wa vyama vya upinzani, wanaharakati na viongozi kadhaa wa dini.

Ni jambo lililo dhahiri kuwa viongozi wa jumuiya hii wanamkumbatia Mugabe, wanayafumbia macho maovu anayofanya dhidi ya wananchi wake kwa kisingizio cha kupambana na maadui wake wa kisiasa, ambao pia ni Wazimbabwe kama yeye.

Sababu kubwa ya kumkumbatia Mugabe ni ile ile, ya huyu ni mwenzetu, tumetoka naye mbali.

Lakini cha ajabu katika hilo ni kwamba, viongozi hawa wanasahau kuwa hata hao Wazimbabwe walio katika mateso makali kutoka utawala wa Mugabe, nao ni wenzao, walipigania uhuru pamoja, na kwamba Mugabe peke yake, bila kuwapo hao anaowatesa, asingefanikiwa kutimiza ndoto aliyokuwa nayo ya kuung’oa utawala wa kikoloni na kuwa kiongozi wa kwanza wa taifa hilo.

Lakini la kusikitisha zaidi kwa viongozi wa jumuiya hii, Tanzania ikiwa kinara wao, ni pale wanaposhindwa kumwambia ukweli Mugabe, kuwa damu ya wananchi wake wakakti wa kudai uhuru, haikumwangika kwa ajili ya kutafuta mateso anayowapa sasa.

Viongozi wengi wanaounda jumuiya hii nchi zao zimetawaliwa na watu weupe na zimepata uhuru kwa njia ya mtutu wa bunduki, tunajiuliza, hivi hawa wamesahau mateso waliyokuwa wakiyapata msituni wakati wa kudai uhuru?

Tunashangazwa na ukimya wa viongozi hawa dhidi ya vitendo vya Mugabe, ambao unaweza kutafsiriwa kuwa anayofanya Mugabe dhidi ya wana wa Afrika wazaliwa wa Zimbabwe, kwao viongozi hawa, kwa sababu Mugabe ni Mwafrika, ni sahihi.

Hii ina maana kuwa, ni Wazungu tu wanaopaswa kulaaniwa wanapofanya vitendo vinavyokiuka haki za binadamu, lakini kwa Waafrika ni sahihi?

Sisi tunadhani muda wa kumwambia ukweli Rais Mugabe umefika, ili kuepusha aibu inayoweza kuwakuta viongozi wa jumuiya yetu hii wanaoendelea kumkumbatia. Hatutaki Mugabe ang’olewa kwa aibu madarakani na wananchi wake ambao tunaamini wamechoshwa na mateso anayowapa.

Tunatambua kuwa Mugabe na Chama chake cha ZANU - PF ni maswahiba wakubwa wa viongozi walioko madarakani pamoja na vyama wanavyo viongoza.

Lakini pamoja na uswahiba huo, litakuwa jambo la busara walau, wakiyakataa matendo yake, lakini wakaendelea kumpenda, vinginevyo watambue kuwa tafsiri iliyopo sasa ni kwamba, wapigania uhuru wa Afrika waliomwaga damu yao nchini Zimbabwe, waliimwanga ili Mugabe aingie madarakani na kumwaga damu ya Wazimbabwe wenzake.

Chonde chonde, tunawasihi viongozi hawa, wawe wawazi kwa Mugabe kwa ajili ya masilahi ya Wazimbabwe walio wengi ambao sisi sote ni ndugu zetu.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by Kimbembe)
    Rating
    Poor article ive ever red! I think we all have to make analysis of situation in Zimbabwe based on the source of the problems in Zimbabwe.The problem in Zimbabwe started when Cmrd Mugabe redistribute the land owned by few white farmers to the poor majority blacks Zimbabweans,which i think it was a right thing to do for a president of any nation when there is any oppression based on the color.That action caused great critisim from UK and US.We know the member of house of common have shares in those white farms in Zimbabwe,we know they were geting huge benefits from those farms.But nobody care for the poor blacks Zimbabweans who were working tirelessly in the white farms for daily pay check!..Nobody critised the white farmers for their inproper,poor condition and brutality treatment of the poor black Zimbabweans who were working in those farms.This is hipocrisy,stupidity,racism and bullishit for so called opposition leaders like Tsvangirai who we know they are being supported from Downing street and white house.If you author of this article claim to be down with democracy why you dont tell the UK and US government for their attrocities which they have caused to the people of this world.Why we don see the articles critise US or UK for their seggretion policies against black people all over the world.Do you know that currently half of the blacks Americans men in US are in prison? Why we don see your article critise the guantanamo bay and the Irag issue? why we don see any article critise the US government policies toward bad situation in DRC-congo? We know they supported Mobutu for many years and none of these so called democratic people like you said anythin! Do u see the problem which the people of Congo are experiencing? So shut up if you only see Zimbabwe and not other western nation and US
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.