Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Lowassa aomba wataalamu
Lowassa aomba wataalamu
By Habari Tanzania | Published  03/27/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu


WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa, ameiomba serikali ya New Zealand, kutuma nchini mabingwa wa elimu na madini pamoja na wa utengenezaji wa mafuta ya petroli kwa kutumia mazao.

Lowassa, ambaye yuko hapa kwa mkutano wa Umoja wa Serikali za Mitaa wa Jumuiya ya Madola, alitoa ombi hilo katika mazungumzo na Waziri Mkuu wa New Zealand, Helen Clark, akisema kuwa mpango huo utakuwa ni sehemu ya kuendeleza uhusiano na ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.

Alisema kwa vile kuwafundishia Watanzania New Zealand ni gharama kubwa, nchi hiyo inaweza kutuma mabingwa wake nchini na kuweza kuwafundisha watu wengi kwa wakati mmoja.

New Zealand ina ujuzi na uzoefu mkubwa katika maeneo ya elimu, madini, utengenezaji mafuta kwa kutumia mazao, kilimo na mifugo.

Imekuwa ikitoa nafasi chache za masomo kwa Tanzania na misaada ya kiufundi na kiuchumi ambayo New Zealand imo katika mfumo wa misaada inayotolewa na nchi mbalimbali kwa pamoja.

Vile vile, New Zealand, ambayo ni nchi ya Mashariki ya Mbali, husaidia mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali nchini Tanzania.

Mazungumzo ya Lowassa na Clark, yaliyofanyika Ikulu, yalihusu uhusiano na ushirikiano baina ya nchi hizi mbili na hali ya kisiasa Afrika.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa New Zealand alisema nchi yake inafanya mapitio ya mkakati wake wa utoaji misaada kuona uwezekano wa kuongeza misaada zaidi kwa Afrika.

Aliipongeza Tanzania kwa msimamo wake katika medani za kimataifa, hasa jinsi ilivyoiunga mkono New Zealand katika uteuzi wa wagombea wa nchi hiyo katika nafasi za Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola na Jaji wa Mahakama Kuu ya Kimataifa.

Raia wa New Zealand, Donald Mckinnon, alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola katika mkutano mkuu wa Jumuiya hiyo mwaka 1999 na Sir Kenneth James Keith, alichaguliwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Novemba 2005 kuwa Jaji katika Mahakama hiyo ya kimataifa.

Leo, Lowassa atauhutubia mkutano wa Umoja wa Serikali za Mitaa wa Jumuiya ya Madola, akiwa ni mmoja wa viongozi wazungumzaji wakuu katika mkutano huo.

Sherehe za ufunguzi wa mkutano huo zilifanyika jana alasiri katika ukumbi wa kituo cha Aotea Centre mjini hapa, ambako mkutano huo unafanyika.

Lowassa, ambaye ujumbe wake uliwasili mjini hapa Jumapili, jana alipokewa rasmi katika sherehe iliyojumuisha kukagua gwaride na mapokezi ya kimila ya kabila la Wamaori, ambao ndiyo wenyeji wa visiwa vya New Zealand kabla ya kufika Wazungu kutoka Ulaya.

Jana usiku, Lowassa alitarajiwa kuhudhuria karamu ya chakula cha usiku, iliyoandaliwa na mwenyeji wake, Waziri Mkuu Clark kwenye hoteli ya Langham alikofikia.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.