Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Makamba ala kiapo bungeni
Makamba ala kiapo bungeni
By Habari Tanzania | Published  06/20/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Luteni (Mstaafu) Yusuf Makamba aliyeteuliwa na Rais kuwa Mbunge wiki iliyopita, ameapishwa rasmi leo asubuhi.

Mzee Makamba alikula kiapo saa 3:10 kabla ya kipindi cha maswali na majibu.

Mbunge huyo mpya alisindikizwa na wabunge wa mkoa wa Dar es Salaam wakati anatinga ndani ya nyumba.

Pia nje kulikuwa na wawakilishi wawili kutoka Jijini Dar es Salaam waliotumwa rasmi kuleta mashada ya kumpamba.

Wawakilishi hao mmoja ametoka katika ofisi yake ya mkoa wakati mwingine ametoka Kinondoni.

Wakati huohuo teknolojia katika ukumbi mpya wa Bunge ilileta gozi gozi tena kiasi cha ’maiki’ kushindwa kufanya kazi.

Kwa mtaji huo, muuliza swali alilazimika kuhamia sehemu wanayosimama mawaziri ili aweze kusikika.

Tatizo hilo liliathiri pia watalaam wa kurekodi kumbukumbu za Bunge na mjadala unaoendelea Bungeni.

Hadi tunakwenda mitamboni, tatizo hilo lilikuwa linaendelea kutafutiwa ufumbuzi.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Articles to Read' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.