Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Japan yamwaga mabilioni Tanzania
Japan yamwaga mabilioni Tanzania
By Habari Tanzania | Published  03/10/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Jonas Songora

SERIKALI za Tanzania na Japan jana zilitialiana saini mikataba ya mikopo na msaada itakayogharimu jumla ya Sh102.4 bilioni.Utiaji saini huo wa mikataba mitatu tofauti, ulifanyika katika ofisi za Wizara ya Fedha, ambako Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Gray Mgonja, alitia saini kwa upande wa Tanzania na Balozi wa Japan nchini, Makoto Ito, akiiwakilisha nchi yake.

Akizungumza mara baada ya utiaji saini huo, Mgonja alisema mkopo wa muda mrefu wa Yen 600 milioni za Japan, sawa na Sh6.5 bn za Tanzania, utatatumika moja kwa moja katika Mpango wa Kupunguza Umasikini nchini (Mkukuta), fedha ambazo zitaingizwa katika bajeti ya serikali katika mwaka ujao wa fedha.

Aliongeza kuwa mkopo wenye masharti nafuu wa Yen 2 bilioni (karibu sawa na Sh21.7 bilioni) zimetolewa kupitia mfuko wa kusaidia kupunguza umasikini (PSRC) na kufadhiliwa na Benki ya Dunia.

Kati ya fedha hizo, sh74.2 bilioni zimetengwa kwa ajili ya kutengeneza barabara ya Arusha - Namanga. Mgonja alisema barabara hiyoi mepewa umuhimu mkubwa ikizingatiwa kuwa karibu asilimia 20 ya bidhaa zinazosafirishwa na kuingia nchini kutoka Kenya hupitia barabara hiyo itakayojengwa kwa kiwango cha lami.

"Barabara hii itaimarisha uchumi wa nchi na pia kuongezea kipato kwa wakazi waishio kando ya barabara hiyo," alisema Mgonja.

Balozi wa Japan nchini aliyefuatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Japan ya Maendeleo ya Dunia, Koji Tanami, aliahidi nchi yake kuendelea kutoa misaada na mikopo kwa serikali ya Tanzania kutokana na usimamizi mzuri wa fedha hizo.

Hata hivyo alisema serikali yake itasimamia kwa karibu matumizi ya fedha hizo ili ihakikishe kuwa zinatumika kama makubaliano yanavyoanisha na si vinginevyo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.