BAGHDAD
WAZIRI MKUU wa Iraq, Nouri al-Maliki amesema wiki mbili zijazo atafanya mabadiliko ya baraza lake la mawaziri ili kumaliza mgawanyiko wa makundi ya kikabila katika Serikali yake na kuleta umoja wa kitaifa.
Waziri huyo aliliambia shirika la habari la AP kwamba atahakikisha Iraq inafanikiwa na kuwa usalama madhubuti.
Waziri Mkuu huyo, Al-Maliki umekuwa katika wakati mgumu hasa baada ya Marekani kumshinikiza kumaliza mgawanyiko ulioko katika ya serikali iliyowashirikisha Wahiite, Wasunnina Wakurd.
Al- Maliki hakusema ni mawaziri wangapi katika baraza lake watabadilishwa lakini maafisa wa Serikali yake, walisema mawaziri tisa watapoteza kazi, wakiwemo mawaziri sita wa kabila la Shiite ambao wanaipinga Marekani.
Muqtada al-Sadr katika bunge la Iraq, ana viti 30 kati ya viti 275 vya bunge.
Hata hivyo pamoja na al- Sadr kuwa na viti vingi bungeni, Marekani imekuwa ikimshawishi Waziri Mkuu, al-Sadr kuachana na al- Sadr na kuunda muungano mpya wa Washiite, wakimo Wasunni wachache na Wakurd.
Ilielezwa mkutano utakaofanyika wiki ijayo, utawaunganisha Wairaq wote, Iran na Syria pamoja na nchi za magharibi.
Hata hivyo Iran haijathibitisha kama itaudhuria mkutano huo au la lakini Iraq inaamini Tehran itamtuma mwakilishi wake.