Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Bajeti ya SMZ bilioni 214.8
Bajeti ya SMZ bilioni 214.8
By Habari Tanzania | Published  06/20/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mohammed Abdullahman, Zanzibar
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), inatarajia kutumia sh bilioni 214.8 katika bajeti ya mwaka 2006/2007.
 
Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Mambo ya Fedha na Uchumi, Dk. Mwinyihaji Makame, alipozungumza na waandishi wa habari.
 
Akifafanua, alisema sh bilioni 110.35 zinatarajiwa kutumika kwa matumizi ya kawaida na sh bilioni 104.44 kwa matumizi ya mandeleo.
 
Alisema kwamba pato la taifa linatarajiwa kukua kwa asilimia 6.2 kutoka asilimia 5.6 mwaka uliopita.
 
Waziri huyo alitamba kuwa bajeti hiyo imelenga kumkomboa mnyonge kutoka kwenye lindi la umaskini.
 
Alisema kwamba serikali haitapandisha kodi katika vyanzo vyake mbali mbali vya mapato, ili kufanikisha mpango wa serikali wa kupunguza mfumko wa bei za bidhaa mbali mbali.
 
“Serikali katika mwaka ujao wa fedha haikusudii kuongeza kodi katika vyanzo vya mapato, badala yake itaimarisha mkakati wa ukusanyaji mapato,” alisema Dk. Makame.
 
Alisema katika mwaka huu wa fedha kasi ya mfumko wa bei inatarajiwa kupungua kutoka asilimia 9.7 hadi asilimia 8.5
 
Dk. Makame alisema kutokana na kasi ya ukuaji wa uchumi, pato la taifa linatarajiwa kukua kwa asilimia 6.2, iwapo mipango mbali mbali ya maendeleo itafanikiwa kwa kushirikiana na wahisani.
 
Alisema Zanzibar ilikumbwa na misukosuko ya mfumko wa bei, hasa bei ya bidhaa za chakula na mafuta, ambapo mfumko wa bei ulifikia asilimia 9.7 kutoka asilimia 8.1 mwaka 2004.
 
Alisema serikali imepanga kukusanya mapato kutoka katika vyanzo vya ndani sh bilioni 83.17.
 
Katika bajeti hiyo, serikali inatarajia kutekeleza miradi ya maendeleo 39 na programu 13.
 
Dk. Makame alisema katika bajeti iliyopita sehemu kubwa ya mapato ya serikali ilikwenda katika ulipaji wa mishahara na uendeshaji wa shughuli mbalimbali na kupewa kipaumbele zaidi katika sekta za elimu, afya, mawasiliano, uchukuzi, ujenzi, maji, na kilimo.
 
Alisema serikali iliweza kukusanya asilimia 89.34 ya mapato yake katika kipindi cha Julai mwaka 2005 hadi Machi, mwaka huu, ikiwa ni kodi ya ushuru wa forodha na kodi ya mapato.
 
Wananchi wengi wanasubiri serikali itasema nini juu ya masilahi ya watumishi wa umma katika mwaka ujao wa fedha.
 
Katika sherehe za Mei Mosi mwaka huu, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Zanzibar walipendekeza mshahara wa kima cha chini ufikie sh 100,000 kwa mwezi badala ya sh 50,000 za sasa.
 
Bajeti hiyo inatarajiwa kusomwa katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kesho, huku sekta ya biashara ikilalamikiwa kuwa imedorora kwa kiwango kikubwa Zanzibar .
 
 

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.