Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Msimamo wa serikali kuhusu wamachinga haujabadilika
Msimamo wa serikali kuhusu wamachinga haujabadilika
By Habari Tanzania | Published  03/5/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Kizitto Noya

SERIKALI itaendelea kupiga marufuku biashara za kimachinga mitaani na kuwataka wafanyabiashara hao kwenda katika maeneo yaliyotengwa na kujiunga na vikundi vya biashara ili wapewe mikopo ya kuendeleza biashara zao.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Kandoro alisema mwishoni mwa wiki kuwa biashara za mitaani hazina tija wala mwanga wa maendeleo na zinawafanya wafanyabiashara hao kuendelea kuwa maskini siku zote.

"Mtu anazunguka kutwa nzima na soksi mbili, vitambaa vitatu vya mikononi na maji katuni moja. Hapa atakuwa na maendeleo gani?" alihoji Kandoro.

Kandoro alisema kuwa mpango wa serikali wa kuwataka machinga waende katika maeneo waliyopangiwa umelenga kuwasaidia wafanyabiashara hao kujikomboa na umaskini badala ya kuwaangamiza kama inavyofikiriwa na baadhi ya watu.

Kwa mujibu wa Kandoro, mtu anayetetea machinga waendelee kufanya biashara katika mitaa ya kati kati ya jiji hawatakii mema wafanyabiashara hao kwani kwa kukaa huko hakuna namna serikali ikawafahamu na kuwapa mikopo.

Alisema serikali sasa imekamilisha makubaliano na benki mbalimbali kutoa mikopo kwa wafanyabiashara hao kwa riba nafuu kwa lengo la kuwawezesha kuendeleza mitaji yao na kuondoka na umaskini.

"Wewe ukishabikia machinga abaki barabarani humsaidii, huuangalii hatma yake ya miaka kumi ijayo. Leo anatembea barabarani kwa kuwa ana nguvu akizeeka ataishi vipi?" alihoji Kandoro.

Alisema kwa mujibu wa nadharia ya uchumi, uchumi endelevu unatokana na shughuli za uzalishaji mali tofauti na kazi za kimachinga zinazofanywa bila jitihada za kuzalisha bidhaa zingine. Alisema Machinga wanatakiwa kujifunza kuzalisha mali na kuiendeleza badala ya kutembeza mali iliyokwishazalishwa ili kujiletea maendeleo endelevu


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.