Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mtoto wa miaka 9 aweka rekodi Mlima Kilimanjaro
Mtoto wa miaka 9 aweka rekodi Mlima Kilimanjaro
By Habari Tanzania | Published  03/4/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:
WATOTO wawili wa miaka tisa na 11, raia wa China, wamefanikiwa kupanda mlima Kilimanjaro hadi kileleni. Mlima wa Kilimanjaro una urefu wa mita 5,895, imefahamika. Watoto hao ndugu ambao ni wanafunzi wa shule ya msingi, Zhang Muyuan(9) na Zhang Muyao(11), waliupanda mlima huo Februari 22 mwaka huu wakiwa na kundi la watu wazima.

Kwa mujibu wa gazeti moja mjini Beijing, watoto hao wamevunja rekodi ya kuwa watoto wadogo kuweza kuupanda mlima huo wakimzidi mtoto wa miaka 12 wa Kimarekani aliyewahi kufika kileleni mwa mlima huo.

Kabla ya kuupanda mlima Kilimanjaro, watoto hao waliupanda mlima Siguniang uliopo nchini China wenye urefu wa mita 5,025. Muyao alisema wamekuwa wakifanya mazoezi ya kupanda kwenye barafu iliyo ngumu. Kwa sasa wanajiandaa kuupanda mlima Jaya ambao pia ni mrefu. Muyao aliwaeleza waandishi wa habari kuwa baada ya kufanikiwa kufika kileleni, alianguka na kufikiria angefariki dunia. Hata hivyo kundi la watu wazima aliofuatana nao walimuokoa.

Hata hivyo wakazi wa China wamepinga kitendo cha mtoto huyo wa miaka tisa kuupanda mlima Kilimanjaro. Mwalimu wa jimbo la Zhejiang, Lin Weiping aliandika barua katika gazeti moja la jioni, liitwalo Yangte akilalamika mtoto huyo kuwekwa katika hatari hiyo ya kupoteza maisha na kuhoji nani aliyetoa taarifa za uongo za mtoto huyo ili aruhusiwe kuupanda mlima huo.

Habari za gazeti hilo zimeripoti kuwa taratibu zilizowekwa kwa wapandaji mlima huo kuwa hairuhusiwi mtoto wa chini ya miaka 10 kupanda mlima. Muyuan anatimiza miaka 10 Aprili mwaka huu. Wakati wa kupanda mlima huo alidanganya umri wake.

Afisa Uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa(TANAPA), Catherine Mmbena alisema umri wa chini wa kupanda mlima Kilimanjaro ni miaka 16. Hata hivyo, hakuwa na maelezo juu ya watoto hao kuweza kupanda mlima huo.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by Ras_Twin)
    Rating
    Ni suala la kuanza kujiuliza kuwa hawa watoto walipanda mlima kupitia wapi na walikuwa na escort ya kina nani. Kama Afisa Uhusiano wa Shilika la Hifadhi ya Taifaanasema hakujua ama hana maelezo ya watoto hawa kupanda mlima Kilimanjaro ambao uko chini ya ya Shirika hilo, hapo tunaanza kupata wasiwasi wa takwimu za watu waupandao na kama kila pato la watalii hao huenda serikalini maana kama hawajui kuwa alikuwepo, ni dhahiri kuwa hakupitia katika taratibu za shirika hilo ama kuna watu kwenye shirika ambao wanajinufaisha kwa UZEMBE wa watawala wa shirika hilo.
    Ni aibu kwa Shirika na Taifa kwa ujumla.
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.