Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mechi ya Yanga, Atletico hofu tupu
Mechi ya Yanga, Atletico hofu tupu
By Habari Tanzania | Published  03/2/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Ruhazi Ruhazi

INAWEZEKANA kusema, pambano la Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga na Petro Atletico ya Angola, ni hofu tupu kwani kila moja ina hofu dhidi ya mwenzake.

Kadiri siku zinavyosogea, ndivyo joto la pambano hilo litakalopigwa Jumapili Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, linavyozidi kupanda.

Wakati Yanga ikipiga marufuku wapenzi na mashabiki kuhudhuria mazoezi yake kwa hofu ya kupelelezwa, hadi kufikia jana, taarifa za kuwasili kwa Atletico, zilikuwa siri.

Licha ya Shirikisho la Sola la Angola kuthibitisha ujio wa timu hiyo, si Yanga wala Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) walio na taarifa rasmi ya kuwasili kwa wageni hao.

Florian Kaijage, ambaye ni Ofisa Habari wa TFF, alisema hadi jana mchana, walikuwa hawana taarifa za kuwasili kwa timu hiyo, licha ya kuelezwa itafika.

“Tumewasiliana na viongozi wa soka Angola, wamethibitisha kuja kwa timu hiyo, lakini hawakuwa tayari kusema ni lini na msafara wa watu wangapi,” alisema Kaijage.

Wakati hali ikiwa hivyo kwa timu zote mbili, waamuzi wa mechi hiyo ya Jumapili kutoka Msumbiji, walitarajiwa kuwasili jana jioni.

Mwamuzi wa kati ni Justino Faduco huku wasaidizi wakiwa ni Henriques Langa na Edmundo Xavie Macamo.

Viingilio vya mechi hiyo ni sh 15,000 kwa Jukwaa Kuu, sh 8,000 kwa Jukwaa la Kijani na sh 3,000 Mzunguko.

Ikicheza nyumbani, Yanga inalazimika kupata ushindi mnono kabla ya matokeo ya mechi ya marudiano itakayopigwa wiki mbili baadaye mjini Luanda, Angola.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.