Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Zitto Kabwe atangaza kung’atuka
Zitto Kabwe atangaza kung’atuka
By Habari Tanzania | Published  03/1/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Samuel Mwanga, Maswa

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ametangaza kung’atuka katika wadhifa wake mwaka 2010.

Kabwe alitangaza adhima yake hiyo jana, wakati akiongea na waandishi wa habari katika Hoteli ya Greenbeach mjini Maswa mkoani Shinyanga.

Alisema amefikia uamuzi huo bila kushinikizwa na mtu yeyote na ameamua kutangaza mapema ili kutoa nafasi kwa wanaotaka kugombea nafasi hiyo, ili wajiandae.

Kabwe alisema anatamani kufanya kazi za kitaalamu, hasa zinazohusu taaluma yake baada ya kuwa mwakilishi wa wananchi kwa kipindi cha miaka mitano.

“Tangu nimalize masomo yangu chuo kikuu, ni kipindi cha mwaka mmoja tu niliofanya kazi kisha nikachaguliwa kuwa mbunge, hivyo nina hamu ya kufanya kazi nyingine mbali na hii ya uwakilishi,” alisema Kabwe.

Alisema uamuzi wake wa kuachana na ubunge hauhusuni na masuala ya siasa ambayo iko katika damu yake.

Kabwe alisema kamwe hataachana na siasa bali baada ya kuachana na ubunge, ataendelea kufanya kazi za kuiimarisha CHADEMA ambayo imemfikisha katika mafanikio aliyonayo sasa.

Aliahidi kuendelea kuwatumikia wananchi wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa uaminifu na kushirikiana nao kuondoa kero mbalimbali zinazowakabiri pamoja na kutimiza ahadi zake alizozitoa wakati wa kuomba kura.

Kabwe alionya kuwa kazi ya ubunge si lelemama kama baadhi ya watu wanavyofikiria, bali ni ngumu na inayohitaji uvumilivu wa hali ya juu.

“Nimeifanya kazi hii ya ubunge kwa muda wa mwaka mmoja sasa, si kazi ya lelemama, ni lazima ujitolee kweli kuwatumikia watu, kwani kila tatizo linapotokea jimboni wananchi wanakutazama wewe mbunge,” alisema Kabwe.

Kabwe ni miongoni mwa wabunge vijana wa CHADEMA ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa vyama vingi wa mwaka 2005 alifanikiwa kuwashinda wagombea wa vyama vingine vya siasa.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.