Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kimataifa  »  Wakamatwa kwa mlipuko wa treni India
Wakamatwa kwa mlipuko wa treni India
By Habari Tanzania | Published  02/25/2007 | Habari za Kimataifa | Unrated

DELHI
POLISI nchini India imesema inawashikilia watu watatu wanaodaiwa kuhusika na ulipuaji wa treni ya abiria ya Samjhauta (Friendship) Express) iliyokuwa ikitokea India kuelekea Pakistan.

Watu wasiopungua 68 Jumapili iliyopita walifariki dunia katika ajali ya moto iliyotokea katika treni hiyo, wengi wao wakiwa ni raia wa Pakistan

Wanaume wawili na mwanamke mmoja walikamatwa Kaskazini mwa Rajasthan kufuatia polisi wa nchi hiyo kupewa taarifa na msamaria mwema.

India ilisema itashirikiana na Pakistan katika kufanya uchunguzi wa kuwasaka watu walihusika katika mlipuko uliosababisha mauaji ya watu hao.

Polisi walisema watu hao walikamatwa katika Wilaya ya Bikaner mpakani mwa Pakistan na wilaya hiyo.

Polisi wanaendelea na uchunguzi na hakuna taarifa sahihi nani alihusika na shambulio hilo lililotokea kilometa 80 kutoka mji wa Delhi.

Hata hivyo polisi walitoa picha za watu wawili ambao walipanda katika treni hiyo muda mfupi kabla haijalipuliwa.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.