Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Meneja NHC kortini kwa kuvunja, kuiba
Meneja NHC kortini kwa kuvunja, kuiba
By Habari Tanzania | Published  02/24/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Tausi Ally

MENEJA wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) mkoani Tabora, Damas Ngoiya (47), mkazi wa Dar es Salaam, Eliaisa Keenja (37) na mfanyabiashara, Josephati Nyambekwa, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, wakikabiliwa na mashitaka matatu likiwamo la kuvunja nyumba na kuiba.

Akisoma hati ya mashitaka, mbele ya Hakimu Adolf Mahay, Kamishna wa Polisi, Charles Kenyela, alidai kuwa katika shitaka la kwanza, watuhumiwa hao kwa pamoja walikula njama ya kutenda kosa la wizi wa Sh333.3 milioni mali ya Li Jinjlan.

Katika shitaka la pili, Kenyela alidai kuwa Mei 9, mwaka jana, majira ya saa 11.00 jioni, watuhumiwa hao walivunja nyumba namba 103 iliyopo katika barabara ya Haile Selasie jijini Dar es Salaam Kitalu namba 3579 ambayo ni mali ya Shirika la Nyumba (NHC) iliyokuwa imepangwa na Jinjlan na kufanya wizi huo.

Katika shitaka la tatu, watuhumiwa hao wanadaiwa kuiba bandari 74 za nguo, digital camera mbili, simu moja ya mkononi aina ya Nokia, kitanda kimoja cha mbao, kabati tano za mbao na moja la chuma, vipande vya madini aina ya almasi, vito vya Tanzanite na Rubi vyote vikiwa na thamani ya Sh333.3 milioni mali ya Jinjlan.

Watuhumiwa hao walikana mashitaka na upande wa mashitaka ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Hakimu Mahay aliwataka watuhumiwa hao kila mmoja awe na wadhamini watatu ambao watasaini bondi ya Sh20 milioni na hati za nyumba ili waweze kupata dhamana. Aliiahirisha kesi hiyo hadi Machi 9, itakapotajwa.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.