Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Jengo la Kitega Uchumi chupuchupu
Jengo la Kitega Uchumi chupuchupu
By Habari Tanzania | Published  06/18/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Jengo la Kitega Uchumi lililopo Jijini Dar es Salaam, limenusurika tena kuungua baada ya majiko ya mgahawa wa Chinese uliopo pembeni yake, kulipuka moto.

Tukio hilo lilitokea juzi usiku na kusababisha hofu kubwa kwa wapangaji kikiwemo kituo cha Radio Clouds Fm.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Bw. Alfred Tibaigana, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 3:30 usiku.

Kamanda Tibaigana alifafanua kuwa, chanzo cha majiko ya mgahawa huo kulipuka na kusababisha moshi mwingi kutanda eneo hilo ni baada ya vyakula vilivyokuwa vikipikwa kuachwa kwa muda mrefu vikichemka kwenye mafuta.

Alisema kitendo hicho cha kuacha vyakula kwa muda mrefu kwenye mafuta, kilisababisha majiko kulipuka na moto wake ukatanda katika sehemu ya jengo hilo huku moshi ukitanda jengo la kitega uchumi.

Hata hivyo, Kamanda Tibaigana alisema moto huo uliozimwa na askari wa Kikosi cha Zimamoto cha Halmashauri ya Jiji, haukuleta madhara yoyote kwa binadamu wala mali zilizokuwemo ndani yake.

Baadhi ya watu walioshuhudia tukio hilo, waliiambia Nipashe Jumapili kuwa, tukio hilo lilisababisha kituo cha Radio Clouds Fm kukatisha ghafla matangazo yake kwa takriban dakika 30.

Jengo hilo limekuwa mara kwa mara likipatwa na ajali za moto kutokana na sababu mbalimbali.

Katika tukio la kwanza, jengo hilo lenye ofisi za makampuni, mashirika na makazi ya watu, lilishika moto Aprili, mwaka 2002 ambapo mali yenye thamani ya Sh. 891, 809, 225 zikiwemo za kituo cha Radio Clouds Fm.

Aidha, Desemba, 2004, jengo hilo lilishika moto tena ulioanzia katika ghorofa ya nne kwenye makazi ya mpangaji mmoja na kuenea hadi ghorofa ya sita na saba.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.