Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Waziri, RC waumbuana mbele ya Waziri Mkuu
Waziri, RC waumbuana mbele ya Waziri Mkuu
By Habari Tanzania | Published  02/20/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu

MKUU wa Mkoa (RC) wa Dar es Salaam, Abbas Kandoro jana alimshushia tuhuma nzito, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Margaret Sitta, kuwa wizara yake imekuwa ikitoa taarifa za uongo dhidi ya pesa za ujenzi wa shule.

Alisema watendaji katika wizara hiyo, wana tabia ya kuwadanganya walimu wakuu wanaofuatilia pesa za ujenzi wa shule kuwa tayari zipo na wanaonyesha mgawo ulivyo katika karatasi, lakini wanapotakiwa kuzikabidhi, zinakosekana.

Kandoro aliyasema hayo jana mbele ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ambaye alikuwa katika ziara ya siku moja kuangalia ujenzi wa shule za sekondari jijini Dar es Salaam.

“Tumechelewa kukamilisha ujenzi wa shule kwa sababu upatikanaji wa pesa kutoka wizarani kupitia Mpango wa Elimu ya Sekondari (MMES), ni tatizo.

“Watendaji wa wizarani wana tabia ya kuwadanganya walimu, wanawaonyesha makaratasi kuwa pesa ziko tayari, lakini wakiziomba zinakuwa hazipo,” alisema Kandoro.

Hata hivyo, kabla hajamaliza, Waziri Sitta alimkata kauli na kueleza kuwa kauli yake si ya kweli, kwa sababu Mkoa wa Dar es Salaam Hazina ipo karibu, hivyo shule zinawahi kupata pesa.

Baada ya maelezo hayo ya Sitta, waziri mkuu, alimwita Mratibu Msaidizi wa MMES, Alpius Machagge na kumtaka atoe ufafanuzi kuhusu mgongano wa kauli za vigogo hao.

Machagge alimweleza Lowassa kuwa, pesa hizo zinawasilishwa mashuleni mara moja baada ya kutoka Hazina.

Kandoro aliipinga kauli ya Machagge na kumweleza Lowassa kwa kumkumbusha kuwa hata alipokuwa Temeke, alimsikia mkuu wa wilaya akilalamika kwamba ujenzi wa shule nane umechelewa kwa sababu ya kuchelewa pesa za MMES.

Katika hali ambayo haikutarajiwa na wengi, Waziri Sitta aliingilia kati na kueleza kuwa Mkoa wa Dar es Salaam umejichelewesha kwa kupeleka majina ya sekondari ambazo hazijasajiliwa, ndio maana walishindwa namna ya kuwapelekea pesa hizo.

Malumbano hayo yalikatishwa na Machagge ambaye aliomba kuonana na Kandoro ofisini kwake ili kulizungumzia suala hilo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.