Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wanaorudia mitihani ya darasa la saba kuanza kesho
Wanaorudia mitihani ya darasa la saba kuanza kesho
By Habari Tanzania | Published  02/20/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:
na Nasra Abdallah

WANAFUNZI waliofutiwa matokeo yao ya mtihani wa darasa la saba mwaka jana, wanatarajia kuanza kufanya marudio ya mitihani hiyo kesho.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa, Joyce Ndalichako alisema mitihani hiyo itafanyika kwa siku mbili.

“Kutokana na taarifa ya tume iliyochunguza tuhuma za udanganyifu katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi Septemba 2006, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilibatilisha matokeo ya watahiniwa 1,857 ambapo walipewa fursa ya kurudia mtihani,” alisema.

Ndalichako alisema, orodha ya watahiniwa wanaopaswa kurudia mtihani wa kumaliza elimu ya msingi inapatikana kwa maafisa elimu wote wa mikoa na wilaya husika na katika shule zote zilizokuwa na watahiniwa waliositishiwa matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2006.

Alisema lengo la wizara ni kuhakikisha kuwa, wanafunzi wanaorudia mtihani ambao watafaulu wanapata fursa ya kuchaguliwa kujiunga na elimu ya Sekondari kabla ya Machi 15 mwaka huu. Matokeo yao yatatolewa Machi 4.

Mikoa yenye mtihani wa marudio ni Arusha, Dodoma, Kagera, Kilimanjaro, Mara, Mtwara, Mwanza, Shinyanga, Tabora na Mbeya.

Kutokana na udanganyifu wa mtihani wa darasa la saba uliofanyika mwaka jana, Januari 26 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Margaret Sitta alitangaza kuwavua vyeo baadhi ya maafisa elimu na walimu wakuu ambao maeneo yao yalionekena kuhusika kwa namna moja au nyingine katika udanganyifu huo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by Joseph Alfred)
    Rating
    is good news for me
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.