Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Fundi saa akutwa na kichwa cha mtoto 'ofisini'
Fundi saa akutwa na kichwa cha mtoto 'ofisini'
By Habari Tanzania | Published  02/19/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated

Doris Mageta

MKAZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, mkoani Rukwa, Amani Mwakisyala, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini Sumbawanga kwa kosa la kukutwa na kichwa cha binadamu kwenye eneo lake la kazi.

Akisoma shitaka hilo Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Cleophas Mpinge, alieleza mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Arcad Chuwa, kuwa mshitakiwa Mwakisyala ambaye ni fundi saa alikutwa na kichwa cha mtoto anayedhaniwa kuwa na umri kati ya miaka miwili na mitatu February 9, mwaka huu, majira ya saa 7:00 mchana katika eneo
lake la kazi kwenye Soko Kuu la mjini Sumbawanga, huku akiwa anaendelea na shughuli zake.

Hata hivyo, Mwakisyala amekana shtaka hilo na kurudishwa Rumande kwa kushindwa kupata wadhamini wawili wa Sh300,000 kila mmoja
wao.

Taarifa za awali za polisi zilidai kuwa mshitakiwa alikutwa na kichwa hicho kikiwa kenye mfuko wa rambo, ambapo alitarajia kukiuza kwa mteja wake kwa thamani ya Sh600,000, lakini kabla hajatimiza azma hiyo polisi hilo kwa kushirikiana na raia wema waliandaa mtego na kufanikisha kumkamata mtuhumiwa akiwa ameweka kifurushi hicho chenye kichwa cha mtu, chini ya meza yake ya ufundi.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Dhamin Zongo, kichwa hicho kimehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali Mkoa.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.