Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Homa ya Bonde la Ufa yapuuzwa Kilimanjaro
Homa ya Bonde la Ufa yapuuzwa Kilimanjaro
By Habari Tanzania | Published  02/19/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Daniel Mjema, Moshi

WATEJA wa nyama na wauzaji wa kitoweo hicho mkoani Kilimanjaro, wameanza kuingiza mzaha katika suala la kujikinga na ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa, kwa madai kuwa wataalamu hawasemi ukweli kuhusu ugonjwa huo.

Uchunguzi wa gazeti hili katika maeneo mbalimbali mjini hapa, umebaini kuwa siku
za mwanzo watu wengi walichukua tahadhari na kuacha kutumia kitoweo hicho, lakini kadri siku zinavyoenda hali inaendelea kubadilika.

Baadhi ya baa na hoteli ambazo zilifuta kabisa '_nyama choma'_ sasa wamerudisha upya kwa madai kwamba kinachotakiwa ni nyama iive vizuri kwa kutumia joto la nyuzi joto 60 na kuendelea.

_"Hapa kuna kitu serikali inatuficha, kama wanasema hao waliokufa walikula nyama, ina maana mtu mmoja tu alikula ng'ombe mzima mwenye kilo zaidi ya 200 peke yake? " alihoji mchinja nyama mmoja wa hapa.

Mchinja nyama huyo anayemiliki mabucha kadhaa ya kuuza nyama, alihoji waliko watu wengine waliokula nyama hiyo na kuiomba serikali itoa ufafanuzi katika suala hilo vinginevyo (wachinjaji) hawataielewa.

Meneja wa baa mashuhuri ya Oysterbay Executive iliyopo karibu na soko la Mbuyuni, mjini hapa, Bayi Nderemo, aliiomba Serikali kutoa elimu zaidi juu ya ugonjwa huo kuliko ilivyo sasa ambapo wananchi wanachanganyikiwa.

"Kuna maneno mengi yanazungumzwa juu ya ugonjwa huo, hivyo ni jukumu la serikali kusema waziwazi kwamba ni wakati gani nyama ikiliwa haitakuwa na madhara na inatakiwa ichemshwe au ichomwe kwa kiwango gani," alisema Nderemo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.