Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mkapa awa Mkuu wa Chuo Kikuu Dodoma
Mkapa awa Mkuu wa Chuo Kikuu Dodoma
By Habari Tanzania | Published  02/18/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Mwandishi Wetu

RAIS Jakaya Kikwete amemteua rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu kipya cha serikali kinachojengwa Dodoma.

Kikwete, pia amemteua aliyekuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dk Mohammed Gharib Bilal kuwa mwenyekiti wa baraza la chuo hicho kitakachoanza rasmi Septemba mwaka huu.

Waziri wa Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Petter Msolla alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa kuanzishwa kwa chuo hicho ni sehemu ya jitihada za serikali kukabiliana na changamoto ya ongezeko la wanafunzi wenye sifa za kujiunga na vyuo vya elimu ya Juu nchini.

"Rais, pia amemteua Profesa Idris Kikula kuwa Makamu wa Mkuu wa chuo kikuu cha Dodoma na Profesa Ludovick Kinabo kuwa Naibu Makamu Mkuu wa chuo hicho anayeshughulikia taaluma, utafiti na ushauri," alisema Msolla.

Aidha, alisema kuwa Profesa Shaaban Mlacha ameteuliwa kuwa Naibu Makamu wa chuo anayeshughulikia fedha, mipango na utawala


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.