Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Marekani yakiwezesha kiwanda kuzalisha umeme
Marekani yakiwezesha kiwanda kuzalisha umeme
By Habari Tanzania | Published  02/16/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Mwasu Sware.

SHIRIKA la Biashara na Maendeleo la Marekani limetoa kiasi cha Sh401 milioni kwa Kampuni ya Sukari ya Kilombero ili kuiwezesha kutumia taka kuzalisha umeme.

Akizungumza na waandishi jana, Balozi wa Marekani nchini, Michael Retzer, alisema umeme utakayozalishwa utatumika katika uendeshaji wa kiwanda hicho na kuchangia kwenye gridi ya Taifa.

Retzer alisema hivi karibuni Kampuni hiyo inatarajiwa kuanza kuzalisha ethani (ethanol) inayotokana na taka kwa ajili ya kuuza katika soko la nje.

"Hivi sasa kampuni ya Sukari itaanza kuzalisha ethani kwa ajili kuuza katika soko la nje, hivyo tatizo la wapi taka hizo zipelekwe litakuwa limeepukika na uzalishaji wa kiwandani utaimarika na kiwango cha uzalishaji wa nishati kitaongezeka," alisema Retzer.

Alisema teknolojia mpya ya uzalishaji wa ethani kutoka kwenye taka na uzalishaji wa nishati ya umeme zitajenga mustakabali wa usimamizi mzuri wa kutunza mazingira na kuimarisha uchumi.

Naye Meneja wa Kiwanda cha Sukari Kilombero, Dave Coates, alieleza kuwa kutokana na msaada huo, kiwanda kitaweza kuzalisha kwa uhakika na kuinua uchumi wa nchi.

Coates alisema, kiwanda hicho kama kikizalisha vizuri, kitachangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa uchumi wa nchi, kuongezeka kwa ajira na wakulima wa miwa kupata soko la urahisi kwa bidhaa zao.

Alisema kwa sasa kiwanda hicho kina takribani wafanyakazi 5,000 na wakulima wapatao 7000 ambao wanawategemewa na kiwanda hicho katika uzalishaji wa Sukari.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.