Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  JK: Mambo mazuri yaja
JK: Mambo mazuri yaja
By Habari Tanzania | Published  06/17/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Mishahara kupandishwa ni mwanzo tu
 
Na Maura Mwingira, Babati
 
RAIS Jakaya Kikwete, amewaahidi Watanzania kwamba mambo mazuri yanakuja, baada ya kuboresha mishahara ya watumishi wa umma katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha.
 
Akihutubia kwenye mkutano wa hadhara mjini hapa jana, kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa Rais wa Jamhuri, Rais Kikwete alisema maboresho yatakuwa mazuri zaidi, baada ya kukamilika kazi ya tume aliyounda kupitia mishahara ya watumishi wa umma na kutoa mapendekezo.
 
Rais aliahidi kutekeleza ahadi alizotoa kwenye kampeni, akisema kwamba ni za kweli, hazikuwa danganya toto na kwamba Watanzania si mabwege wa kudanganywa, kwani wameamka.
 
Aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania, ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma za kijamii na kuweka mazingira mazuri ya kujiajiri na kujiongezea kipato. Alisisitiza ujenzi wa barabara kwa lami kutoka Minjingu hadi Singida kuanza mwaka huu wa fedha na barabara ya kutoka Babati - Kondoa - Dodoma na ile itakayounganisha makao makuu ya mkoa yenye urefu wa kilometa 250.
 
Akigeukia rushwa na tabia mbaya za watumishi wa umma, Rais Kikwete alisema hakuna maelezo sahihi ya kuielezea rushwa, zaidi ya kuwa rushwa ni "haramu haramu haramu!" na kuongeza kuwa, watumishi wengi wa umma wamekuwa wakiomba na kupokea rushwa kwa kisingizio kwamba mishahara wanayopata ni midogo na haikidhi haja.
 
Rais alisema kuna watumishi wanaotekeleza majukumu yao kana kwamba hawajaenda shule, kwa kutoa uamuzi unaokwenda kinyume cha taaluma zao, na kuwalazimisha wananchi kutoa rushwa kwa huduma wanazotakiwa wazitoe bure. Alisema ataendelea kuwakumbusha kutekeleza wajibu kwa kuzingatia taaluma walizosomea.
 
Alisisitiza kwamba, ifike mahali watumishi wa umma waachane na tabia ya kuwaambia wananchi 'nenda rudi kesho' bila kutoa majibu sahihi, akaongeza kwamba watumishi wote wa umma wako katika nafasi zao za kazi kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na kusukuma maendeleo yao .

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.